Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Real Madrid yaweka Pauni 120 Bilioni kwa Diomande

MADRID Pict

Muktasari:

  • Nyota huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 19 anatarajiwa kuwa mmoja wa usajili mkubwa zaidi wa majira haya ya kiangazi, huku ada hiyo ikimfanya kuwa miongoni mwa wachezaji ghali zaidi kuwahi kusajiliwa na miamba hiyo ya Hispania.

MADRID, HISPANIA: REAL Madrid imefikia makubaliano ya kumsajili winga chipukizi wa RB Leipzig, Yan Diomande, katika dili linaloweza kufikia euro 140milioni  (takribani Pauni milioni 120), baada ya mazungumzo ya muda mrefu kati ya klabu hizo.

Nyota huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 19 anatarajiwa kuwa mmoja wa usajili mkubwa zaidi wa majira haya ya kiangazi, huku ada hiyo ikimfanya kuwa miongoni mwa wachezaji ghali zaidi kuwahi kusajiliwa na miamba hiyo ya Hispania.

Diomande amekuwa akifuatiliwa kwa karibu na Real Madrid kutokana na kiwango chake bora akiwa RB Leipzig, ambapo ameonyesha uwezo mkubwa wa kucheza pembeni kwa kasi, ubunifu na uwezo wa kufunga mabao.

MADRI 01

Endapo dili hilo litakamilika rasmi, Real Madrid itakuwa imeongeza silaha nyingine muhimu kwenye safu yake ya ushambuliaji, ikiendelea na mkakati wa kusajili vipaji bora vya dunia kwa ajili ya kujenga kikosi cha muda mrefu.

MADRI 02
MADRI 02

Wakati huo huo, Liverpool inaendelea kuchunguza uwezekano wa kumsajili mshambuliaji kijana Ibrahim Mbaye, huku Aston Villa ikiripotiwa kufikia makubaliano ya kumsajili beki wa kushoto Matteo Ruggeri, katika harakati za kuimarisha vikosi vyao kabla ya kuanza kwa msimu mpya.