Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

PSG yalenga historia mpya Ulaya

Muktasari:

  • Mabingwa hao wa Ulaya kwa misimu miwili mfululizo wana nafasi ya kuwa timu ya pili katika historia kutwaa Ligi ya Mabingwa Ulaya mara tatu mfululizo.

PARIS, UFARANSA: Paris Saint-Germain (PSG) inaanza msimu mpya ikiwa na lengo lilelile ililotumia kumaliza msimu uliopita kutwaa taji la Ulaya.

Mabingwa hao wa Ulaya kwa misimu miwili mfululizo wana nafasi ya kuwa timu ya pili katika historia kutwaa Ligi ya Mabingwa Ulaya mara tatu mfululizo.

Hata hivyo, safari yao inaanza kwa mchezo wa UEFA Super Cup dhidi ya Aston Villa, mabingwa wa Europa League, leo Jumatano mjini Salzburg, Austria.


WANATAKA KUINGIA HISTORIA

Baada ya miaka mingi ya kusubiri na kutumia mabilioni ya fedha katika usajili, PSG hatimaye ilitwaa Ligi ya Mabingwa mwaka 2025.

Mwaka huo iliichapa Inter Milan mabao 5-0 katika fainali iliyochezwa Munich, kabla ya msimu uliofuata kuifunga Arsenal kwa penalti mjini Budapest na kutwaa tena taji hilo.

Kabla yao, Real Madrid ndiyo ilikuwa timu pekee iliyowahi kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa mara mbili mfululizo, ikifanya hivyo mara tatu mfululizo kati ya 2016 na 2018.

Hata timu kubwa zilizowahi kutawala soka la Ulaya kama Barcelona ya Pep Guardiola, Manchester City, Manchester United ya Sir Alex Ferguson na baadhi ya vikosi bora vya Bayern Munich hazikufanikiwa kutwaa taji hilo mara tatu mfululizo.

Sasa kocha Luis Enrique na PSG wanataka kuifikia rekodi hiyo ya Real Madrid.

Kwa ujumla, ni timu tatu pekee zilizowahi kutwaa Kombe la Ulaya mara tatu mfululizo: Real Madrid, iliyoshinda mataji matano ya kwanza kati ya 1956 na 1960, Ajax na Bayern Munich, ambazo zilifanya hivyo katika miaka ya 1970.

Ikiwa rekodi itaongezeka hadi kushinda mataji matatu ndani ya miaka mitano, Liverpool nayo inaingia kwenye orodha hiyo baada ya kutwaa mataji mwaka 1977, 1978 na 1981.

PSG YALENGA KUFAGIA MATAJI YOTE


PSG itashiriki mashindano sita msimu huu, matatu kati yake yakiwa ni fainali za mchezo mmoja, na inaingia ikiwa miongoni mwa timu zinazopigiwa nafasi kubwa ya kushinda kila taji.

Mashindano hayo ni UEFA Super Cup, Trophée des Champions, Ligi ya Mabingwa, Ligue 1, Kombe la Ufaransa na FIFA Intercontinental Cup.

Msimu uliopita PSG ilitwaa mataji matano, rekodi ambayo inalingana na idadi kubwa zaidi iliyowahi kushinda kwa msimu mmoja, ikishindwa pekee katika Kombe la Ufaransa baada ya kutolewa na jirani zao Paris FC mwezi Januari.

Msimu mmoja kabla ya hapo, PSG ilitwaa mataji manne.

Hakuna klabu kubwa iliyowahi kutwaa mataji sita makubwa katika msimu mmoja.

Mbali na PSG, rekodi ya kushinda mataji matano katika msimu mmoja inashikiliwa na Celtic, iliyofanya hivyo msimu wa 1966/67, huku timu kadhaa zikiwahi kutwaa mataji manne, zikiwemo Barcelona, Real Madrid, Bayern Munich, Manchester United na Manchester City.

JE, PSG ITAANZA KWA MWENDO WA POLE?

PSG inaweza kuhitaji muda kuingia katika kiwango chake cha juu msimu huu kutokana na kuwa na wachezaji 16 waliokwenda Kombe la Dunia.

Wachezaji sita kati yao walifikia hadi wiki ya mwisho ya mashindano hayo; watano wakiwa sehemu ya kikosi cha Ufaransa na Fabian Ruiz akiwa na mabingwa Hispania.

Wachezaji wanane wa PSG walifunga angalau bao moja katika Kombe la Dunia, rekodi kwa klabu moja katika historia ya mashindano hayo.

Tatizo ni kwamba kuna siku 24 pekee kati ya fainali ya Kombe la Dunia na UEFA Super Cup, hivyo baadhi ya wachezaji wanaweza kuanza msimu wakiwa hawajapata muda wa kutosha wa kupumzika.

Msimu uliopita pia PSG haikuanza kwa utulivu baada ya kuwa na mwezi mmoja pekee kati ya fainali ya Kombe la Dunia la Klabu na Super Cup.

Katika Super Cup, ilianza kwa kufungwa 2-0 na Tottenham kabla ya kusawazisha na hatimaye kushinda kwa penalti baada ya sare ya 2-2.

PSG pia imekuwa na mwanzo wa taratibu katika Ligi ya Mabingwa katika misimu ya hivi karibuni, ikilazimika kucheza mechi za mtoano baada ya kushindwa kumaliza ndani ya timu nane bora katika hatua ya ligi, kabla ya kuimarika na kwenda kushinda taji.


MABADILIKO MACHACHE KIKOSINI

PSG imekuwa na kikosi kinachofanana kwa kiasi kikubwa katika misimu miwili iliyopita.

Katika fainali mbili za mwisho za Ligi ya Mabingwa, ilianza na wachezaji wale wale 10 wa uwanjani, huku mabadiliko pekee yakitokea katika nafasi ya kipa.

Wachezaji hao 10 bado wapo klabuni.

Katika dirisha hili la usajili, PSG hadi sasa imewaongeza kiungo wa Monaco, Maghnes Akliouche, beki wa kushoto wa Aston Villa, Lucas Digne, na kipa wa miaka 18 kutoka AC Milan, Alessandro Longoni.

Walioondoka hadi sasa ni Lee Kang-in, aliyejiunga na Atletico Madrid, na Goncalo Ramos, aliyehamia AC Milan.

Mshambuliaji Bradley Barcola naye anaweza kuondoka na kujiunga na Liverpool kwa ada inayokadiriwa kufikia pauni milioni 100.

Wachezaji hao wote watatu walikuwa kwenye benchi katika fainali ya Ligi ya Mabingwa.

PSG ilijaribu pia kumsajili mshambuliaji wa Leipzig na Ivory Coast, Yan Diomande, lakini ofa yao ya pauni milioni 102.5 ilikataliwa. Mchezaji huyo baadaye alijiunga na Real Madrid kwa dili linaloweza kufikia pauni milioni 120.

Kwa sasa, PSG inaonekana kuelekeza nguvu zake katika kumsajili mshambuliaji wa Barcelona, Ferran Torres, ambaye alifunga bao pekee la Hispania dhidi ya Argentina katika fainali ya Kombe la Dunia.

Kwa Luis Enrique na PSG, msimu mpya unaonekana kuwa na malengo mawili makubwa: kuendelea kutawala Ulaya na kuandika historia ambayo haijawahi kufikiwa na klabu nyingi.