Carrick aongoza orodha ya kutimuliwa
Muktasari:
- Carrick alishuhudia kikosi chake cha Manchester United kikipata kipigo cha kusikitisha cha mabao 2-0 dhidi ya Hull City Jumamosi.
MANCHESTER, ENGLAND: MICHAEL Carrick amekuwa kocha anayefikiriwa zaidi na kampuni za kubashiri kuwa ndiye atakayekuwa kocha wa kwanza wa Ligi Kuu England kutimuliwa msimu huu.
Na kwa mujibu wa kampuni moja ya ubashiri, tayari kuna kocha anayependekezwa zaidi kuchukua nafasi yake endapo ataondoka Manchester United.
Carrick alishuhudia kikosi chake cha Manchester United kikipata kipigo cha kusikitisha cha mabao 2-0 dhidi ya Hull City Jumamosi.
Licha ya United kumiliki mpira kwa kiwango kikubwa, walionyesha kiwango duni katika maeneo yote ya mchezo na kushindwa kuzuia timu hiyo mpya kwenye Ligi Kuu kupata ushindi muhimu.
Hali hiyo imezua maswali kuhusu mustakabali wa Carrick, hasa kutokana na ukweli kwamba United waliingia msimu huu wakiwa na matumaini makubwa.
Baada ya kumaliza msimu uliopita kwa nguvu, United walifanya usajili wa wachezaji wapya na pia walikuwa na maandalizi mazuri ya msimu mpya.
Hata hivyo, kikosi hicho bado kinaonekana kuwa na mapungufu katika baadhi ya maeneo, hasa kutokana na jukumu la kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.
United pia walionekana kuwa na ratiba nzuri ya kuanza msimu, wakikutana na Hull City na Ipswich katika michezo yao miwili ya kwanza kabla ya kusafiri kwenda kukutana na Everton katika mchezo wa tatu.
Kwa hiyo, kipigo dhidi ya Hull Jumamosi kimeanza kupiga kengele za tahadhari, hali ambayo imeonekana pia kwenye masoko ya ubashiri.
Betfair imeshusha odds za Carrick kuwa kocha wa kwanza wa Ligi Kuu England kutimuliwa kutoka 33/1 hadi 6/1, jambo lililomfanya awe kinara wa sasa kwenye soko hilo.
Carrick amewapita Frank Lampard na Sergej Jakirović, ambao wote wamepewa odds za 7/1.
Orodha ya makocha wanaoweza kutimuliwa
Michael Carrick – 6/1 (kutoka 33/1)
Sergej Jakirović – 7/1
Frank Lampard – 7/1
Roberto De Zerbi – 17/2 (kutoka 16/1)
Álvaro Arbeloa – 17/2
Gary O’Neil – 9/1
Oliver Glasner – 9/1
Enzo Maresca – 12/1
Unai Emery – 12/1 (kutoka 50/1)
Matthias Jaissle – 12/1
Régis Le Bris – 12/1
Pierre Sage – 16/1
Eddie Howe aibuka kama mrithi wa Carrick
kampuni hiyo pia imeweka odds za makocha wanaoweza kuchukua nafasi ya Carrick endapo Manchester United itaamua kumtimua.
Aliye mbele kwa mbali ni Eddie Howe, aliyekuwa kocha wa Newcastle United.
Howe aliondoka Newcastle msimu wa joto na kuamua kuchukua mapumziko kutoka kwenye ukocha, lakini sasa amewekwa kama chaguo kubwa la kuchukua nafasi ya Carrick Old Trafford.
Nyuma yake kwenye soko hilo ni Julian Nagelsmann, mwenye odds za 10/3, huku Thomas Tuchel akiwa na odds za 4/1.