Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Arsenal yatuma salamu za msimu mpya

ARSENAL Pict

Muktasari:

  • Kwa muda wa miaka mitatu, Manchester City ilikuwa imejenga hofu ndani ya Arsenal, huku kikosi cha Mikel Arteta kikishindwa kuvuka kikwazo cha mwisho na mara kwa mara kumaliza nyuma ya mabingwa hao.

LONDON, ENGLAND: Arsenal imeonyesha dalili zote za kuwa timu yenye nguvu zaidi katika soka la England baada ya kuonyesha kiwango cha juu, ubora na kina kuelekea msimu mpya.

Kwa muda wa miaka mitatu, Manchester City ilikuwa imejenga hofu ndani ya Arsenal, huku kikosi cha Mikel Arteta kikishindwa kuvuka kikwazo cha mwisho na mara kwa mara kumaliza nyuma ya mabingwa hao.

Hali hiyo sasa imebadilika. Baada ya Arsenal kutwaa ubingwa wa Premier League msimu uliopita, Gunners wameanza kuonyesha sura mpya ya timu isiyohofia wapinzani na iliyo tayari kutumia nafasi ya kuwa kileleni kutawala kwa muda mrefu.

Katika mchezo wao wa ngao dhidi ya Manchester City, Arsenal haikuonyesha dalili za kuridhika baada ya kupata bao. Badala yake, kila bao liliongeza hamu ya kutafuta jingine, jambo linaloonyesha mabadiliko makubwa ndani ya kikosi hicho.

ARS 03

ODEGAARD AWA KIONGOZI

Nahodha Martin Odegaard alikuwa mmoja wa wachezaji walioonyesha zaidi mabadiliko hayo.

Baada ya msimu uliopita kukumbwa na majeraha mbalimbali ya goti na bega yaliyomfanya akose mwendelezo wa kucheza, kiungo huyo wa Norway alirejea akiwa na ari kubwa ya kuthibitisha thamani yake.

Odegaard alicheza kwa kujiamini, akitawala eneo la kiungo, akitoa pasi za kupenya safu ya ulinzi na pia kufanya presha kubwa kwa wapinzani.

Bao lake dakika ya 48 lilikuwa kilele cha kiwango chake, akiwazidi ujanja Josko Gvardiol na Gianluigi Donnarumma kwa kutumia miguso mitatu pekee kabla ya kufunga.

Ilikuwa ni aina ya uchezaji wa nahodha halisi, huku Odegaard akionyesha kwa nini Arteta bado anaamini kwake licha ya kuwepo kwa mjadala wa Declan Rice kupewa kitambaa cha unahodha.

Arteta alisema Odegaard alikumbwa na kipindi kigumu msimu uliopita kutokana na kukaa nje kwa miezi kadhaa, lakini akiamini akiwa fiti na akizungukwa na wachezaji sahihi, atakuwa mchezaji tofauti kabisa.

ARS 02

KIKOSI KIPANA

Arteta pia alitoa ujumbe mwingine kupitia mabadiliko yake ya kikosi.

Baada ya Arsenal kutawala mchezo, alimwingiza Declan Rice kipindi cha pili, kabla ya Bukayo Saka na Piero Hincapie kuingia dakika ya 60.

Hatua hiyo inaonyesha Arsenal sasa ina kikosi chenye uwezo wa kubadili mchezo bila kupunguza ubora wa timu.

Kwa kifupi, Gunners wanaonekana kuwa na kikosi kipana kinachoweza kuwafanya wapinzani wapate wakati mgumu pindi timu hiyo inapocheza katika kiwango chake bora.

Na huku timu nyingine za kile kinachoitwa ‘Big Six’ zikiwa katika kipindi cha mabadiliko, Arsenal inaonekana kuwa na nafasi nzuri ya kuendelea kutawala.

ARS 06

TZOLIS NI SILAHA MPYA

Mchezaji mwingine anayevutia ni Christos Tzolis, ambaye kwa kiasi fulani amekuwa nje ya uangalizi kutokana na Arsenal kuhusishwa zaidi na kutafuta winga mkubwa wa bei.

Tzolis, mwenye umri wa miaka 24 na aliyesajiliwa kwa pauni milioni 34 kuchukua nafasi ya Leandro Trossard, tayari ameanza kuonyesha kuwa huenda akawa moja ya usajili bora wa Arsenal.

Alitoa pasi ya kichwa iliyomsaidia Kai Havertz kufunga baada ya kumponyoka beki, huku pia akitoa pasi sahihi iliyomweka Odegaard katika nafasi ya kufunga.

Mchango wake umefikia mabao sita yaliyohusika moja kwa moja kufunga au kutoa asisti katika michezo sita ya maandalizi ya msimu.

Hiyo inaonyesha wazi kuwa Tzolis hataki kuwa mchezaji wa benchi pekee. Anataka nafasi katika kikosi cha kwanza na, iwapo Arsenal haitasajili winga mwingine ghali kabla ya dirisha la usajili kufungwa, nafasi yake inaweza kuwa kubwa zaidi.


KINA GABRIEL WAZUA MASWALI

Kutokuwepo kwa Ethan Nwaneri, Gabriel Martinelli na Gabriel Jesus katika kikosi pia kulizua mjadala.

Nwaneri amekuwa akihusishwa kutakiwa na klabu mbalimbali, huku Martinelli akiripotiwa kuwa amewindwa na Galatasaray kwa ofa ya pauni 38 milioni.

Kwa upande wa Jesus, dalili zinaonyesha kuwa anaweza kuwa karibu zaidi na kuondoka, huku Napoli ikihusishwa na uhamisho wake.

Hata hivyo, Arteta alipunguza uzito wa suala hilo, akisema uteuzi wa kikosi haukuwa na uhusiano na wachezaji hao kuondoka klabuni.

Kocha huyo alieleza kuwa kanuni za mashindano zinawaruhusu kuingiza wachezaji 18 pekee wa uwanjani na kwamba walichagua kikosi walichoona kinafaa zaidi kwa mchezo huo, hasa kutokana na hali ya kimwili ya baadhi ya wachezaji.

Pamoja na maelezo hayo, kutokuwepo kwa nyota hao watatu kumeongeza hisia kwamba Arsenal inaweza kuwa inajiandaa kufanya mabadiliko zaidi ndani ya kikosi.