Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Arsenal yakamilisha dili la Konsa

FUNUNU Pict

Muktasari:

  • Konsa, 28, anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Arsenal na kuanza maisha mapya Emirates.

Arsenal imefikia makubaliano na Aston Villa kumsajili beki wa kimataifa wa England, Ezri Konsa, kwa ada inayozidi Pauni 50 milioni.

Konsa, 28, anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Arsenal na kuanza maisha mapya Emirates.

Arsenal ilifungua tena mazungumzo na Aston Villa wiki iliyopita kuhusu usajili wa Konsa, lakini wakati huo klabu hizo zilishindwa kufikia makubaliano.

Kutokana na hali hiyo, Arsenal ilionekana kuhamishia nguvu zake kwa beki Jarell Quansah wa Bayer Leverkusen, kabla ya kurejea tena kwenye mpango wa kumsajili Konsa.

Safari hii, Arsenal imefanikiwa kufikia makubaliano na Villa na sasa ipo hatua za mwisho kukamilisha usajili huo.

Konsa alijiunga na Aston Villa Julai 2019 na katika misimu yake saba akiwa na klabu hiyo amecheza jumla ya mechi 286.

Msimu uliopita alikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Unai Emery, akicheza mechi 48 katika mashindano yote, akifunga mabao mawili na kutoa asisti moja.

Konsa hajashiriki katika mchezo wowote wa maandalizi ya msimu wa Aston Villa, ikiwemo kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Paris Saint-Germain katika mchezo wa UEFA Super Cup.

Kocha Emery alimpa mapumziko ya wiki nne baada ya Konsa kushiriki Kombe la Dunia akiwa na England.


Ollie Watkins

Aston Villa imekataa ofa ya Al Hilal ya euro milioni 45 kwa ajili ya mshambuliaji Ollie Watkins. Klabu hiyo ya Saudi Arabia bado inamuhitaji Mwingereza huyo, 30, lakini msimamo wa Villa unaweza kuzuia dili hilo. Watkins pia anakabiliwa na ushindani wa nafasi baada ya kuwasili kwa mshambuliaji Tammy Abraham msimu huu.


Ismaila Sarr

Crystal Palace imekataa ofa ya Galatasaray ya kumsajili winga Ismaila Sarr, ikimtambua Msenegal huyo kama sehemu muhimu ya mipango yake. Palace iko tayari kumuuza kwa ofa kubwa pekee. Sarr alifunga mabao tisa na kutoa asisti moja katika mechi 28 za Ligi Kuu msimu uliopita, akisaidia klabu kufuzu Conference League.


Lutsharel Geertruida

Sunderland inakaribia kumpoteza beki Lutsharel Geertruida baada ya kufikia makubaliano ya kumpeleka kwa mkopo PSV Eindhoven, kwa mujibu wa Fabrizio Romano. Dili hilo lina kipengele cha PSV kumnunua moja kwa moja baada ya mkopo. Thamani ya kipengele hicho inakadiriwa kuwa karibu pauni milioni 13, hivyo Geertruida anaweza kuondoka kabisa Sunderland.



Bradley Barcola

Liverpool imeanza kusukuma dili la kumsajili winga wa Paris Saint-Germain, Bradley Barcola, lakini bado kuna tofauti kubwa kuhusu thamani yake. PSG inataka pauni milioni 145, wakati Liverpool iko tayari kutoa karibu pauni milioni 120. Tofauti ya pauni milioni 25 imekuwa kikwazo kikubwa katika mazungumzo ya klabu hizo mbili.


Jack Grealish

Everton inaamini Jack Grealish yuko tayari kurejea Merseyside msimu huu baada ya kufanya vizuri alipokuwa kwa mkopo msimu uliopita. Mwingereza huyo alianza vyema katika kikosi hicho, kabla ya kupata jeraha la mguu Januari lililomweka nje hadi mwisho wa msimu. Everton sasa inatumaini kurejea kwake kunaweza kuimarisha safu yao ya ushambuliaji.


Omar Marmoush

Tottenham Hotspur imeongeza nguvu katika harakati za kuwasajili mastaa wawili wa Manchester City, Omar Marmoush na Savinho, kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Spurs wanataka kuwakamilisha wachezaji hao kwa pamoja ili kuongeza ubora wa kikosi. Mazungumzo yanaendelea huku klabu hiyo ikitafuta makubaliano yanayoweza kufanikisha usajili wao mapema.


Harry Kane

Mshambuliaji wa Bayern Munich, Harry Kane, amesema hamu yake ya kurejea England ili kuvunja rekodi ya Alan Shearer ya mabao 260 ya Ligi Kuu imepungua. Kane, aliyeondoka Tottenham mwaka 2023, amefunga mabao 213 kwenye ligi hiyo, akihitaji mengine 47 kufikia rekodi ya Shearer. Amesema hamu hiyo si kubwa tena.


Tijjani  Reijnders

Kiungo wa kimataifa wa Uholanzi, Tijjani Reijnders, amekamilisha uhamisho wa kujiunga na Al-Qadsiah ya Saudi Arabia kwa pauni milioni 52. Reijnders, 28, anaondoka Manchester City mwaka mmoja baada ya kujiunga akitokea AC Milan kwa pauni milioni 46.5. Msimu uliopita alicheza mechi 50, akifunga mabao saba katika mashindano yote.


Curtis Jones

Inter Milan iko hatua za mwisho kumnasa kiungo wa Liverpool, Curtis Jones, kwa ada ya euro milioni 35. Mabingwa hao wa Italia wamefikia makubaliano ya awali na Liverpool. Awali, Reds walikataa ofa ya euro milioni 25. Jones, 25, amebakiza mwaka mmoja mkatabani, jambo linaloweza kurahisisha dili hilo kukamilika.