Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Vigogo Ulaya katika mtihani mzito

Muktasari:


  • Mbali ya timu nane za juu ambazo tayari zimeshafuzu kucheza 16 bora, kuanzia timu ya tisa hadi 24, zitacheza mechi mbili nyumbani na ugenini ili kutafuta nane nyingine zitakazokwenda 16 bora.

MADRID, HISPANIA: BAADA ya jana kumalizika kwa hatua ya ligi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, vigogo mbalimbali barani humo wamejikuta katika mtihani wa kucheza mechi za mtoano kuwania kufuzu hatua ya 16 bora ya michuano hiyo baada ya kumaliza katika nafasi za chini.

Mbali ya timu nane za juu ambazo tayari zimeshafuzu kucheza 16 bora, kuanzia timu ya tisa hadi 24, zitacheza mechi mbili nyumbani na ugenini ili kutafuta nane nyingine zitakazokwenda 16 bora.

Droo ya mechi hizo inatarajiwa kufanyika kesho huko Nyon, Uswisi kuanzia saa 8:00 mchana.

Bingwa mtetezi Real Madrid ambayo imemaliza katika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi hiyo, kwenye hatua ya mtoano inaweza kukutana na aidha Celtic au Manchester City na ikishinda kwenda 16 bora itakuwa na uwezekano wa kuumana na Atletico Madrid na Bayer Leverkusen sawa na Bayern Munich ambayo pia inaweza kukutana na Man City au Celtic.

Vilevile PSG inaweza kupangwa na Monaco au Brest na ikipita inaweza kukutana na kati ya Liverpool au Barcelona kwenye 16 bora.

Kwa upande mwingne AC Milan na PSV Eindhoven zinaweza kuumana na Feyenoord na Juventus na mmoja wao akipita anaweza kuumana na Arsenal au Inter Milan.

Baada ya droo ya kesho, mechi za mkondo wa kwanza zinatarajiwa kupigwa kuanzia Februari 11 hadi 12 kisha za mkondo wa pili zitaanza Februari 18 hadi 19.

Baada ya hapo itafanyika droo ya robo fainali, Februari 21, baada ya kumaliza kwa mechi hizo za mtoano na kupatikana kwa timu nyingine nane zitakazoungana na nane zilizofuzu moja kwa moja.


HATUA YA MTOANO:

KILA TIMU ITAKUTANA NA MOJA YA TIMU HIZI: 

Atlanta: Sporting Lisbon au Club Brugge

Borussia Dortmund: Sporting Lisbon au Club Brugge

Real Madrid: Celtic au Man City

Bayern Munich: Celtic au Man City

AC Milan: Feyenoord au Juventus

PSV: Feyenoord au Juventus

PSG: Monaco au Brest

Benfica: Monaco au Brest

Feyenoord: AC Milan au PSV

Juventus: AC Milan au PSV

Celtic: Bayern Munich au Real Madrid

Manchester City: Bayern Munich au Real Madrid

Sporting Lisbon: Atalanta au Borussia Dortmund


Club Brugge: Atalanta au Borussia Dortmund


HATUA YA 16-Bora:


Liverpool: PSG, Benfica, Monaco au Brest


Barcelona: PSG, Benfica, Monaco au Brest

Arsenal: AC Milan, PSV Eindhoven, Feyenoord au Juventus

Inter Milan: AC Milan, PSV Eindhoven, Feyenoord au Juventus

Atletico Madrid: Real Madrid, Bayern Munich, Celtic au Man City

Bayer Leverkusen: Real Madrid, Bayern Munich, Celtic au Man City

Lille: Atalanta, Borussia Dortmund, Sporting Lisbon au Club Brugge

Aston Villa: Atalanta, Borussia Dortmund, Sporting Lisbon au Club Brugge