Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mzigo wa Real Madrid, Atletico ni kesho usiku

MADRID Pict

Muktasari:

  • Atletico inatafuta kushinda taji hilo kwa mara ya nne, huku Los Blancos wakilenga kulitwaa kwa mara ya 14 katika historia yao.

JEDDAH, SAUDI ARABIA: BALAA hilo. Mahasimu Atletico Madrid na Real Madrid, watarudisha uhasama wao wa jadi watakapokutana katika nusu fainali ya Spanish Super Cup itakayopigwa Alhamisi hii huko Jeddah, Saudi Arabia.

Atletico inatafuta kushinda taji hilo kwa mara ya nne, huku Los Blancos wakilenga kulitwaa kwa mara ya 14 katika historia yao.

Atletico inaweza kuwa haijapoteza mechi tano mfululizo za mashindano, lakini walihisi kukatishwa tamaa baada ya sare ya 1-1 dhidi ya Real Sociedad, Jumapili iliyopita uwanjani Reale Arena.

Alexander Sorloth alifungua ukurasa wa mabao dhidi ya klabu yake ya zamani katika dakika ya 50, lakini bao lake la tano la La Liga msimu huu lilifutwa haraka na Gonçalo Guedes, hali iliyowalazimu Atletico kukubali sare inayowaacha nafasi ya nne, wakiwa nyuma kwa pointi 11 dhidi ya vinara Barcelona.

Kutokana na hilo, matumaini halisi ya Atletico kushinda ubingwa wa ligi kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2020–21 yanaonekana kufifia katikati ya msimu wa La Liga.

MADRI 01

Hii ina maana kwamba Spanish Super Cup, Copa del Rey na Ligi ya Mabingwa Ulaya yatakuwa muhimu zaidi iwapo hawatataka kumaliza miaka mitano bila taji.

Kikosi hicho cha kocha Diego Simeone kimeshinda nusu fainali moja tu kati ya tatu katika mfumo wa timu nne, mafanikio hayo yakitokea mwaka 2020 walipoifunga Barcelona 3-2 kabla ya kupoteza kwa mikwaju ya penalti dhidi ya Real Madrid kwenye fainali.

Tangu hapo, wamepoteza nusu fainali dhidi ya Athletic Bilbao na Real Madrid mwaka 2022 na 2024 mtawalia, hali inayoonyesha kuwa wanakabiliwa na kazi ngumu ili kufuzu fainali dhidi ya Barcelona au Athletic wiki hii.

Hata hivyo, Los Colchoneros wanaweza kupata faraja kutokana na uzoefu wa dabi ya Madrid ya hivi karibuni mwezi Septemba, ambapo Julián Álvarez alifunga mabao mawili katika ushindi wa kihistoria wa 5-2 dhidi ya Real Madrid kwenye Uwanja wa Metropolitano, ikiwa ni mara ya kwanza kwa Atletico kufunga mabao matano dhidi ya wapinzani wao wa jiji hilo kwa karibu miaka 75.

Kocha wa Real Madrid, Xabi Alonso, amepunguza presha iliyokuwa ikimkabili baada ya mfululizo wa ushindi mara nne, ikiwamo ushindi mkubwa wa 5-1 dhidi ya Real Betis siku ya Jumapili nyumbani, licha ya kumkosa Kylian Mbappe aliyejeruhiwa.

MADRI 02

Mshambuliaji Gonzalo Garcia aling’ara katika nafasi ya Mbappe, akifunga kwa mguu wa kulia, mguu wa kushoto na kichwa, na kuwa mchezaji mdogo zaidi kufunga hat-trick kamili katika La Liga katika karne ya 21, akiwa na umri wa miaka 21 na siku 286.

Real Madrid, waliopigwa vikali na Barcelona kwenye fainali ya Spanish Super Cup msimu uliopita, wamelinyakua taji hilo mara tatu kati ya misimu sita ya mfumo wa timu nne, mara ya mwisho ikiwa mwaka 2024 walipowafunga Atletico 5-3 baada ya muda wa nyongeza kabla ya kuichapa Barcelona 4-1 kwenye fainali.

Hata hivyo, Real Madrid inaweza kuwa na wasiwasi kidogo kutokana na ukweli kwamba wameifunga Atletico ndani ya dakika 90 mara moja tu katika mechi saba za hivi karibuni, na hawajawahi kutoruhusu bao dhidi yao tangu ushindi wa 2-0 nyumbani Desemba 2021.

Atletico Madrid bado wanawakosa Clement Lenglet na Nicolas González, ambao wataendelea na matibabu ya majeraha ya goti na msuli wa paja mtawalia nchini Hispania, wakati Los Blancos haitakuwa na Mbappe, Eder Militao, Brahim Díaz na Trent Alexander-Arnold.


VIKOSI VINAVYOTARAJIWA

Atletico Madrid: Oblak; Llorente, Pubill, Le Normand, Hancko; Simeone, Gallagher, Koke, Baena; Sorloth, Álvarez

Real Madrid: Courtois; Valverde, Huijsen, Rudiger, Carreras; Camavinga, Tchouameni; Rodrygo, Bellingham, Vinícius; García