Fifa yazifungia Kenya, Zimbabwe
Muktasari:
- Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) limeifungia Kenya kushiriki shughuli za soka kutokana na Serikali ya nchi hiyo kuingilia shughuli za michezo. Serikali ya Kenya iliingilia utendaji wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo, FKF.
Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) limeifungia Kenya kushiriki shughuli za soka kutokana na Serikali ya nchi hiyo kuingilia shughuli za michezo. Serikali ya Kenya iliingilia utendaji wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo, FKF.
Rais wa Fifa, Gianni Infantino amethibitisha uamuzi huo wa kusimamishwa kwa Kenya huku akisema hautaathiri wala kuingilia uchunguzi wowote unaendelea kwa mamlaka za nchi hiyo.
Mbali na Kenya, Infatino pia amesema Shirikisho la Soka Zimbabwe nalo limefungiwa kwa muda kutokana na Serikali kuingilia utendaji wake.