Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga, Simba ulinzi kama wote kwa Mkapa

Yanga, Simba ulinzi kama wote kwa Mkapa

Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema Jeshi la Polisi  limejipanga vyema kiusalama kuelekea kwenye mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga  uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Benjamini Mkapa Dar es Salaam Aprili 30 mwaka huu.

Akizungumzia  na wanahabari  leo Alhamisi 28, 2022 Kamanda huyo alisema  wamejipanga kuimarisha ulinzi huo ndani na maeneo jirani  kuhakikisha watu wote wanazingatia sheria na taratibu za mchezo wa soka katika kuingia na kutoka.

“Tunatambua mchezo unavuta hisia kali. Vitu vyote vinavyohusiana na silaha za moto na zisizo silaha za moto ikiwemo visu, mapanga,chupa makopo havitaruhusiwa kuingizwa au kuwekwa sehemu za mashabiki,”alisema

Amesema wanaweka usalama huo kwakutambua uzito kutokana na utani uliopo kwa timu hizo hivyo wamejipanga kuona wote wanaangalia mechi kati mazingira salama.

Amesema Jeshi hilo halitakuwa na msamaha kwa mtu yeyote atakayeonekana kujihusisha na vitendo vya vurugu au kikundi huku akiwaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa fiche za kiarifu na kwamba jeshi hilo litatunza siri na kuwashughulikia watakaokuwa na nia hiyo.