Ruvu kutambulisha nane wapya
KLABU ya Ruvu Shooting imejitapa kesho kutangaza wanajeshi wake 25 watakao ingia kambini kujiweka sawa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania bara.
Ruvu walimaliza nafasi ya 11 katika msimu uliomalizika wakiwa na alama 41 wamesema katika wachezaji watakao watambulisha kutakuwa na maingizo mapya nane ili kuimarisha kikosi chao.
Akizungumza ma Mwanaspoti Afisa habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire anasema baada ya klabu yao kukamilisha usajili wa msimu 2021/2022 kesho watataja majina ya wachezaji wote watakao kuwa nao kueleke msimu huo.
"Suala la usajili kulingana na maitaji ya kocha umekamilika na tunategemea kesho kutangaza kikosi chetu na lini wataingia kambini rasmi kujianda na msimu", amesema Masau.
Imeandikwa na Lilian Mukulu