Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mwambusi hana maisha marefu Yanga

WAZEE wa kudodosa wamepenyeza kuwa eti kocha mpya wa Yanga, Sebastien Migne anaweza kumpiga chini Juma Mwambusi mwishoni mwa msimu mara baada ya kuzoeana na wachezaji.

Chanzo kimoja cha ndani kimenipenyezea kuwa Migne amekubali kufanya kazi na Mwambusi kwa sababu ya uhitaji wake wa kuwasoma wachezaji mastaa na si vinginevyo.

Uoga wa Migne ni kuhujumiwa, hivyo anataka kuweka sawa mipango yake ili ahusike moja kwa moja mwenyewe, lakini hilo linaweza kubadilika kwa mujibu wa chanzo.