Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ajibu kupigwa chini msimbazi

NYOTA wa Simba, Ibrahimu Ajibu huenda akaonyeshwa mlango wa kutokea mwishoni mwa msimu kama asipoonyesha mabadiliko yoyote, maana inaelezwa kiwango chake hakimvutii kocha wa timu hiyo, Didier Gomes.

Habari za ndani zinaeleza kuwa uamuzi huo unaweza kuwaumiza baadhi ya viongozi wa timu hiyo kutokana na mapenzi makubwa waliyonayo kwa mchezaji huyo.

Kuna kipindi Ajibu alisepa Simba na kwenda Yanga, baada ya kufanya vizuri huko na kupewa unahodha, vigogo hao inaelezwa walishinikiza kurejeshwa kwa mtoto wao huyo ambaye ni zao la timu ya vijana ya wekundu.