Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Musonye: Yanga bure kabisa

Musonye

Muktasari:

Cecafa waliamua kuiondoa Yanga katika michuano hiyo iliyoanza jana Ijumaa mjini Kigali, Rwanda baada ya kuwasilisha kikosi chenye wachezaji 13 kutoka kikosi chao cha vijana huku wachezaji wazoefu wakiwa saba pekee tena waliokuwa wakisugua benchi msimu uliopita.

Musonye azidi kukerwa na Yanga

MWANDISHI WETU

KATIBU Mkuu wa Cecafa, Nicholaus Musonye, amekerwa na kikosi alichokiita cha kipuuzi kilichopelekwa na Yanga kwenye michuano ya Kagame kabla hawajakipiga chini.

Cecafa waliamua kuiondoa Yanga katika michuano hiyo iliyoanza jana Ijumaa mjini Kigali, Rwanda baada ya kuwasilisha kikosi chenye wachezaji 13 kutoka kikosi chao cha vijana huku wachezaji wazoefu wakiwa saba pekee tena waliokuwa wakisugua benchi msimu uliopita.

Musonye aliwaambia waandishi wa habari mjini Kigali kwamba ilichofanya Yanga ni upuuzi.

“Yanga ya Tanzania wameamua kutuvuruga, kupuuza na kudharau michuano hii kwa kuleta kitimu cha hovyohovyo kisichokuwa na maana. Tumekataa tumesema tokeni na timu yenu, nendeni mkacheze popote pale mnapotaka huko kwenu Dar es Salaam.”

Kutokana na Yanga kutimuliwa, Azam imepewa nafasi.