Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mlandege yaanza kusuka kikosi

MLANDEGE Pict

KATIBU Mkuu wa Mlandege, Hussein Ahmada amesema dirisha hili kubwa la usajili wameacha wachezaji 15 lakini wana mpango wa kusajili wengine kwa lengo la kukijenga kikosi chao upya.

Kiongozi huyo amesema wachezaji hao wameshawapa barua, pia kuna waliowauza na waliomaliza mikataba.

Hussein amesema, wachezaji walioachwa na waliouzwa idadi yao inafika 15 hadi sasa na hakuna mabadiliko yoyote, kilichobaki sasa ni kuanza kutambulisha majembe mapya.

“Tunataka kutengeneza timu yetu upya, kwa hiyo tutasajili wachezaji wenye uzoefu na uwezo ambao watakwenda na kasi ya Mlandege na si vinginevyo,” amesema.

Katibu huyo amesema, uongozi umeanza mchakato wa kukijenga upya kikosi chake kuelekea msimu mpya baada ya kuwaacha wachezaji 15 katika dirisha kubwa la usajili.

Amesema, uongozi wa klabu tayari umeanza kusajili wachezaji wapya watakaongeza ushindani ndani ya kikosi, huku utambulisho wao ukitarajiwa kufanyika hivi karibuni.