Mbeya Kwanza yavuta kifaa Nkana
KLABU ya Mbeya kwanza FC imefanikiwa kumsajili Salum Abdallah Chuku kutoka Nkana Red Devil FC ya nchini Zambia kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Siku chache zilizopita wageni hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao tayari wamethibitisha usajili wa mchezaji Habibu Haji Kyombo, Mtanzania aliyekua anachezea Mamelody Sundowns Ya Afrika Kusini kwa mkopo.
Pia tayari wamenasa saini ya Rolland Msonjo mlinzi wa kati ambaye ni mchezaji Wa Timu Ya Taifa Ya Vijana (U23) Kwa mkataba wa miaka miwili pamoja na Mizah Cristom Abdallah akitokea Namungo FC.
Aidha pia klabu hio ilimtambulisha Harerimana Haruna raia wa Burundi kuwa Kocha Mkuu atakayeinoa timu hiyo msimu ujao.
IMEANDIKWA NA LEONARD MUSIKULA (TUDARCO)