Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Manchester United yampa presha Cantona

Muktasari:

  • Nahodha wa zamani wa Manchester United, Eric Cantona amesema muda si mrefu mashabiki wa klabu hiyo wataacha kutaja jina lake jukwaani.

London, England. Nguli wa zamani wa Manchester United Eric Cantona amesema ana hofu mashabiki wa klabu wataacha kutaja jina lake uwanjani.

Mashabiki wa Man United wanamuona Cantona ni mchezaji mwenye mafanikio baada ya kuiongoza vyema alipokuwa nahodha.

Licha ya kuondoka Man United miaka 23 iliyopita baada ya kustaafu soka akiwa na kiwango bora, Cantona amekuwa akihusudiwa zaidi na mashabiki wa klabu hiyo.

Mashabiki wa klabu hiyo wamekuwa wakilitaja jina lake katika mechi za timu hiyo jukwaani sanjari na kuweka mabango ya picha zake.

Katika kipindi cha miaka minne na nusu aliyocheza Man United chini ya Sir Alex Ferguson, Cantona (53) aliipa mataji manne ya Ligi  Kuu na mawili ya Kombe la FA.

“Najivunia, naona fahari lakini nina hofu ipo siku mashabiki wataacha kutaja jina langu,”alisema nguli huyo.

Kauli ya Cantona imekuja kipindi ambacho Man United haifanyi  vizuri katika mechi za mashindano mbalimbali tangu alipostaafu Ferguson mwaka 2013.