Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kocha Sheha aahidi makubwa Uhamiaji

SHEHA Pict

KOCHA MKUU wa timu ya Uhamiaji, Sheha Khamis amepanga kufanyakazi kwa umakini ili kusimamia malengo mapya ya msimu wa 2026-2027.

Amesema, anatumia uzoefu wake kuijenga timu hiyo kuwa na ushindani kwa kuleta ladha tofauti kwenye Ligi Kuu ya Zanzibar msimu mpya unaotarajiwa kuanza hivyo karibuni.

Kocha Sheha amesema, kwa sababu viongozi hao wameamua kumuamini kwa kumkabidhi kikosi cha timu hiyo anaahidi kutowaangusha. “Kwasasa kikosi kinajifunza mbinu za kuhakikisha wanafanya vizuri katika mechi zao kwa kujijenga kwa pamoja na ushirikiano,” amesema

Kocha huyo amesema, anachohitaji kutoka kwa wachezaji hao ni ushirikiano na umakini wao kwa lengo la kuitengeneza Uhamiaji anayoitaka.

Amesema, Ligi Kuu ya Zanzibar msimu huu inakabiliwa na mambo mengi hivyo kuna ugumu ndani yake ambao unazilamisha timu kutumia muda vizuri kujiandaa.

Hatahivyo, amesema mpira umekuwa biashara na ajira kwa mantiki hiyo kila mmoja atakuwa tayari kuonesha uwezo wake.

Hivyo, amewasihi wachezaji wa timu hiyo kutokukubali kuachwa nyuma na wengine ni wakati wa kupambania malengo ya timu.