Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

 ‘Mwanzo, Mwisho’ picha la Israel Mwenda, Yanga

MWENDA Pict


YANGA imeweka wazi haijawahi kumsimamisha wala kumwandikia barua ya kumtuhumu beki wake wa kulia, Israel Mwenda kama ambavyo imekuwa ikielezwa kwenye taarifa mbalimbali mitandaoni.


Mwenda hayupo kwenye kikosi cha Yanga kabla ya msimu uliopita kumalizika, huku kuendelea kutoonekana kwake tangu kuanza kwa msimu huu 2026-2027, imezusha taharuki na kila mmoja akihitaji kufahamu alipo beki huyo aliyewahi kuitumikia pia Simba.


Baada ya ukimya huo, ikaelezwa beki huyo alisimamishwa na Yanga kwa madai ya kutuhumiwa kuihujumu timu hiyo katika mechi za Ligi Kuu Bara, hatua ambayo imeuibua uongozi wa mabingwa hao na kuweka wazi.

Akuzungumza na Mwanaspoti, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe amesema madai hayo hayana ukweli na uongozi wa klabu hiyo haukuwahi kumsimamisha Mwenda wala kumtuhumu na jambo lolote.

Kamwe amesema Mwenda mwenyewe ndiye aliyetangulia kukaa nje ya timu bila taarifa na baadaye akaiandikia barua klabu hiyo akiomba kukaa nje ya timu kisha Yanga kuijibu kwa kumtaka kujieleza na kurudi kazini.

MWEND 01

“Hizo taarifa za tumemsimamisha Mwenda sio za kweli hata kidogo, Yanga ni klabu inayofuata utaratibu kwa waajiriwa wake, nimeona sehemu pia wanasema Yanga tulimuandikia barua tukimtuhumu kwamba ameijuhumu klabu, huo nao wote ni uongo,” amesema Kamwe.

“Ukweli ni kwamba kabla ya hata msimu kumalizika, Mwenda alikosekana kwe nye timu tena bahati m baya hakuwa ametoa taarifa yoyote na wa kati huo tu ki wa kwenye presha kubwa ya kuutafuta ubingwa, tulijiuliza na kutafuta aliko tukaambiwa yupo na sisi tulijiridhisha kwamba yupo na hana shida ya kiafya.

MWEND 02

“Wakati ule tukasema tuendelee na vita haukuwa wakati sahihi wa kuanza kutafuta mwanajeshi wako ambaye ameamua kujiondoa vitani, tukaweka akili zetu kwenye kuutafuta ubingwa, tukiendelea na wanajeshi wetu watiifu.

“Baadaye mwezi Julai, uongozi ukapokea barua kutoka kwa Mwenda kwamba ameamua mwenyewe kujiweka kando, tukashangaaa lakini tukamjibu kwamba anatakiwa kurudi kazini na kwenye barua hiyo wala hakuandika haya ambayo yanasemwa sasa.”

Ingawa Kamwe hakutaka kuweka wazi juu ya barua hiyo, lakini Mwanaspoti limejiridhisha baada ya kuinasa barua hiyo iliyoandika Julai 3, 2026, kwenda kwa uongozi wa Yanga ambapo beki huyo aliweka wazi uamuzi wake wa kujiweka pembeni na timu hiyo.

MWEND 03

Katika barua hiyo, imeeleza kwamba beki huyo ameamua kujiweka kando kutokana na kujitathimini kwa kina katika kipindi muhimu ambacho timu hiyo ilikuwa inapambana kufikia malengo yake kutokana na kiwango chake cha wakati huo.

Akizungumzia juu ya kutomlipa mishahara yake, Kamwe amesema Yanga haikuweza kumlipa mchezaji wake ambaye ni mtoro kazini ambapo hatua pekee stahiki waliyofanya ni kujibu barua yake na kumtaka arudi kazini.

“Klabu isingeweza kumlipa mtumishi wake ambaye ni mtoro kazini, alikaa nje bila kutupa taarifa baadaye akaandika barua kwamba ameamua kukaa nje, tukamjibu arudi kazini bahati mbaya hakurudi, hapo unawezaje kuendelea kumlipa huyo mtu, haki inakwenda na wajibu.”

MWEND 04

TATIZO SIMBA

Wakati sakata hilo linafukuta, imefahamika kwamba chanzo cha tuhuma hizo ni beki huyo kutuhumiwa kuihujumu klabu hiyo kwenye mchezo dhidi ya Simba uliopigwa Mei 3, 2026 pale Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Bosi mmoja wa juu wa Yanga amesema baada ya mchezo huo Mwenda alipokea presha kubwa kutoka kwa mashabiki kutokana na makosa ambayo yalitokea kwenye mechi hiyo na kuamua kukaa pembeni.

“Kuna mchezaji anasemwa vibaya kwetu kama Mwamnyeto (Bakari) lakini sisi kama uongozi kuna namna ya kuyafanyia kazi upungufu wa wachezaji wetu, hujawahi kuona Mwamnyeto anachukua uamuzi kama wa Mwenda, aliposakamwa na mashabiki mwenyewe akaamua kukaa pembeni tena bila kutufahamisha,”  amesema bosi huyo wa juu wa Yanga.

MWEND 05

UPANDE WA MWENDA

Alipotafutwa Mwenda kuzungumzia sakata hilo, kupatikana lakini baba mzazi wa beki huyo, Osoro Mwenda, amesema kwasasa hawataki kuendeleza malumbano zaidi ya kutafuta suluhu kati ya klabu hiyo na kijana wake.

Osoro amesema awali alizungumza na Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said juu ya mzozo huo na kukubaliana mambo machache lakini jana (juzi) amepigiwa simu na watu wa serikalini na wadau wa klabu ya Yanga akiambiwa suala hilo linafanyiwa kazi.

“Kwasasa sitaki kuendeleza malumbano, nimekuwa nikizungumza katika kupatikana suluhu ya hizi tofauti, unajua hili tatizo limeanzia mwezi Mei mwaka huu na pande zote mbili zilikuwa kimya. Mimi kama baba nikasema nipulize filimbi ili suluhu ipatikane,” amesema Osoro.

“Baada ya Mimi kuongea nimepokea simu kutoka kwa watu wa serikalini na wadau wa Yanga na hata Israel mwenyewe amenipigia akaniambia kwamba tatizo hili limeanza kushughulikiwa, kwahiyo na mimi nataka kuishia hapa kwasasa.

“Israel ni mtoto wangu wa nne na bado anataka kuendelea na kazi yake kama suluhu itapatikana, bado ana mkataba wa miaka miwili na Yanga, ametumikia mwaka mmoja pekee kwahiyo acha tuone nini kitatokea.”

Akizungumzia hatua ya Yanga kukanusha kumuandikia barua ya kumsimamisha, Osoro amesema;

“Niliongea na Rais wa Yanga (Hersi Said) kuhusu hili la tuhuma hizo lakini bahati mbaya kuna taarifa zinabadilika, niseme kitu kimoja cha muhimu hapa, inawezekana klabu haikumuandikia barua lakini naamini hata nyie waandishi wa habari hizi kelele za tuhuma za kuhujumu zilisikika, hata hii barua ambayo Israel aliandika ilikuwa ni Julai baada ya kuona kuna mambo hayapo sawa.”