Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kelvin John atua Genk

MSHAMBULIAJI chipukizi wa Tanzania, Kelvin John ‘Mbappe’, amejiunga rasmi na klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji ambayo nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta, alikuwa akiichezea kabla ya kujiunga na Aston Villa ya nchini Uingereza.

Kelvin ambaye pia anaichezea timu ya vijana chini ya miaka 20 ya Ngorongoro Heroes ya Tanzania, ni miongoni mwa vijana mwenye kipaji kikubwa kwani Mwaka jana aliorodheshwa na jarida la The The Guardian la nchini Uingereza kuwa miongoni mwa wachezaji wa kizazi kijacho.

Genk imethibitisha kumsajili mchezaji huyo kwa ushauri wa Samatta ambaye amekuwa rafiki yake wa karibu.