Guardiola Mnene aipa neno ZFF
Muktasari:
- Amesema, endapo Ligi ya Vijana itaboreshwa kwa kutafutiwa wadhamini, hilo litaipa nguvu Ligi Kuu Zanzibar na itakuwa sababu ya kuongezeka kwa ushindani.
KOCHA Hassan Makame ‘Guardiola Mnene’ amelishauri Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) kuwekeza ngazi ya vijana kwa lengo la kuviendeleza vipaji vyao.
Amesema, endapo Ligi ya Vijana itaboreshwa kwa kutafutiwa wadhamini, hilo litaipa nguvu Ligi Kuu Zanzibar na itakuwa sababu ya kuongezeka kwa ushindani.
Amesema, mambo hayo yataisaida ZFF kupata uanachama wa FIFA ili Zanzibar ipate nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia.
“Naishauri ZFF wakuze mpira ngazi ya vijana kwa kutafuta wadhamini kuboresha ligi kuanzia vijana hadi Ligi Kuu Zanzibar ili watafute uanachama wa FIFA ili na sisi tupate kushiriki mashindano makubwa kama Kombe la Dunia,” amesema.
Kocha huyo ambaye msimu uliopita alikuwa sehemu ya benchi la ufundi la KVZ iliyotwaa ubingwa wa Ligi Kuu Zanzibar, amesema msimu ujao hatakuwa sehemu ya kikosi hicho.
Amesema, hadi sasa zipo ofa tatu ya timu zinazohitaji huduma yake ingawa hajafanya uamuzi.