Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Makinda ishirini 'wamoto' EPL

MAKINDA Pict

Muktasari:

  • Hawa ni wachezaji 20 wa kuangaliwa ambao iwapo utabahatika kuangalia mechi kati ya timu 20 zinazotarajiwa kuonyesha kazi usiache kuwaangalia wakifanya vitu uwanjani.

LONDON, ENGLAND: ZIKIWA zimebaki takriban wiki mbili kabla ya kuanza kwa msimu wa 2026/27 wa Ligi Kuu England, kuna wachezaji makinda wanaotarajiwa kujitokeza na kuwa na mchango mkubwa katika timu zao na baadhi yao wameanza kupewa nafasi katika timu za wakubwa, huku wengine wakisubiri fursa ya kwanza.

Hawa ni wachezaji 20 wa kuangaliwa ambao iwapo utabahatika kuangalia mechi kati ya timu 20 zinazotarajiwa kuonyesha kazi usiache kuwaangalia wakifanya vitu uwanjani.


Marli Salmon (Arsenal)

Beki huyo mwenye miaka 16 alicheza mara nne Arsenal msimu uliopita na akawa mchezaji wa nne mwenye umri mdogo zaidi kuichezea timu hiyo ya wakubwa. Pia alishinda asilimia 71.8 ya mipambano yake katika PL2 (mashindano ya wachezaji vijana wa Ligi Kuu England). Anaweza kupewa nafasi zaidi na Mikel Arteta msimu ujao.


Brian Madjo (Aston Villa)

Straika huyo mwenye miaka 17 alisajiliwa kutoka Metz kwa takribani Pauni 10.5 milioni. Akiwa na nguvu na umbo kubwa, amevutia katika maandalizi ya msimu na tayari amefunga mabao manne katika mechi za kirafiki.

MAKI 01

Veljko Milosavljevic (Bournemouth)

Beki huyo mwenye umri wa miaka 19 alicheza mechi saba msimu uliopita na sasa anaweza kupata nafasi zaidi baada ya kuondoka kwa Marcos Senesi. Pia amechezea timu ya taifa ya Serbia.


Antoni Milambo (Brentford)

Alisajiliwa kutoka Feyenoord kwa takribani Pauni 21 milioni, lakini msimu uliopita alikumbwa na jeraha la mguu. Kabla ya hapo alikuwa mmoja wa viungo vijana waliofanya vizuri Eredivisie, akihusika katika mabao 14 msimu wa 2024/25.


Zadok Yohanna (Brighton)

Winga huyo wa Nigeria mwenye miaka 19 alisajiliwa kutoka AIK kwa Pauni 21.5 milioni. Aliongoza Allsvenskan kwa majaribio ya chenga, akiwa na wastani wa 8.5 kwa dakika 90. Anaweza kuwa kivutio kipya Brighton.

MAKI 02

Reggie Watson (Chelsea)

Kiungo huyo mkabaji mwenye miaka 16 amevutia kutokana na nguvu, uwezo wa kutumia mpira na uelewa wa nafasi. Analinganishwa kwa tahadhari na Rodri na anaweza kupata nafasi kutokana na changamoto za baadhi ya viungo wa Chelsea.


Kai Andrews (Coventry City)

Kiungo mwenye miaka 19 aliyecheza mechi 10 msimu uliopita kabla ya kwenda Hibernian kwa mkopo. Alianza kwa mara ya kwanza Wales dhidi ya Romania na kufanya vizuri, hivyo anaweza kupewa nafasi zaidi Coventry.


Joel Drakes-Thomas (Crystal Palace)

Alikuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kuichezea Palace Ligi Kuu England msimu uliopita. Alivutia katika Conference League, akitengeneza nafasi na kupiga chenga nyingi. Kuteuliwa kwa Pierre Sage kunaweza kumpa nafasi zaidi.


Tyrique George (Everton)

Baada ya kipindi cha kuzoea Everton, George anaweza kuwa tishio kubwa msimu ujao. Ni mwepesi na mwenye uwezo wa kukabiliana na  mabeki. Ameanza michezo mitatu kati ya minne ya maandalizi ya msimu.

MAKI 03

Farhaan Ali-Wahid (Fulham)

Winga huyo mwenye miaka 19 alifunga mabao 10 na kutoa assists saba katika PL2 msimu uliopita. Ushiriki wake wa mabao 17 ulimweka miongoni mwa vijana waliofanya vizuri zaidi, hivyo anaweza kupewa nafasi ya kwanza Fulham.


Charlie Hughes (Hull City)

Beki huyo alikuwa mhimili wa Hull, akianza mechi 36 za Championship. Alikuwa na rekodi ya kuzuia mara 1.54 kwa dakika 90, nyingi zaidi kwa mchezaji yeyote aliyecheza zaidi ya dakika 1,000. Anaweza kuwa muhimu katika kuipambania ibaki Ligi Kuu England.


Tudor Mendel-Idowu (Ipswich Town)

Winga huyo mwenye miaka 19 alihusika katika mabao 15 kwenye mechi 17 za PL2 msimu uliopita, akifunga tisa na kutoa asisti sita. Kocha Gary O’Neil anaweza kumpa nafasi katika kikosi cha wakubwa.


Jayden Lienou (Leeds United)

Beki huyo mwenye umri miaka 18 alianza karibu kila mchezo wa Leeds katika PL2 msimu uliopita. Alishinda umiliki wa mpira mara 5.4 kwa dakika 90 na pia aliitwa katika kikosi cha Wales.

MAKI 04

Trey Nyoni (Liverpool)

Kiungo huyo mwenye miaka 19 ameonyesha kiwango bora katika maandalizi ya msimu chini ya kocha mpya. Katika mechi tatu za kirafiki nchini Marekani, alikamilisha asilimia 92 ya pasi zake. Anaweza kupata nafasi zaidi katika kikosi cha kwanza.


Ryan McAidoo (Manchester City)

Winga huyo mwenye miaka 18 alifunga katika mechi yake ya kwanza kwa City na ameendelea kuvutia katika maandalizi ya msimu. Ana uwezo mkubwa wa kucheza mmoja dhidi ya mmoja na anaweza kupata nafasi mara kwa mara.


JJ Gabriel (Manchester United)

Ni miongoni mwa vipaji vinavyotajwa zaidi akademi ya Manchester United. Alifunga mabao 23 katika Ligi Kuu England ya U18 msimu uliopita na kushinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu. Anaweza kuwa mmoja wa vijana wa kuvutia zaidi msimu ujao.


Park Seung-soo (Newcastle United)

Winga huyo wa Korea Kusini mwenye umri wa miaka 19 alitumia msimu uliopita kuzoea soka la England. Akiwa na uwezo mzuri wa chenga na kasi, anaweza kunufaika na kuondoka kwa Anthony Gordon.

MAKI 05

Kalum Thompson (Nottingham Forest)

Akiwa na miaka 17, Thompson alikuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi Forest U21 msimu uliopita. Alipiga chenga 4.7 kwa dakika 90 na alihusika katika mabao sita, zaidi ya mchezaji mwingine wa Forest.


Nilson Angulo (Sunderland)

Ingawa ana miaka 23, Angulo bado anaonekana kuwa na nafasi ya kutisha zaidi. Kabla ya kuhamia Sunderland, aliongoza Ligi Kuu Ubelgiji kwa majaribio ya chenga (111) na alikuwa na kuhusika na mabao 11.


Luca Williams-Barnett (Tottenham Hotspur)

Kiungo huyo mshambuliaji mwenye miaka 17 alitoka U18 na kuingia katika mipango ya timu ya kwanza Spurs msimu uliopita. Katika PL2 alikuwa na wastani wa mabao na asisti 1.25 kwa dakika 90, akishika nafasi ya nne kwa wachezaji waliocheza zaidi ya dakika 500. Kwa ujumla, msimu wa 2026/27 unaweza kuwa jukwaa muhimu kwa kizazi hiki cha vijana. Baadhi yao wanahitaji nafasi tu ili kuthibitisha uwezo katika kiwango cha juu.