Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mafundi watatu miguuni na vichwani wamo

MAFUNDI Pict

Muktasari:

  • Hawa ni wachezaji sita wanaolenga kusahau changamoto za msimu uliopita na kurejesha ubora wao, ikizingatiwa kwamba wote ni mafundi miguuni kulicheza boli na pia wazuri vichwani kuamua mechi.

LONDON, ENGLAND: MAISHA katika ligi zote kubwa na ndogo Ulaya yameshaanza upya, na kuna kila dalili kwamba timu zinapishana kuusaka ufalme wa michuano hiyo. Lakini, msimu uliopita baadhi ya wachezaji walipitia kipindi kigumu kwenye Ligi Kuu England, na huu wanaweza kurejea katika viwango  bora na tayari wameshaanza kuonyesha hivyo.

Hawa ni wachezaji sita wanaolenga kusahau changamoto za msimu uliopita na kurejesha ubora wao, ikizingatiwa kwamba wote ni mafundi miguuni kulicheza boli na pia wazuri vichwani kuamua mechi.

Mechi za kwanza za msimu wa 2026/27 tayari zimechezwa, zikitoa picha ya awali kuhusu namna kila timu ilivyojiandaa kwa msimu huu. Muhimu zaidi, mashabiki wameuona pia mwonekano wa kwanza wa wachezaji walioanza msimu kwa kasi.

Kwa baadhi yao, kama Dominik Szoboszlai wa Liverpool na Marc Guehi wa Manchester City, kiwango bora walichoonyesha ni mwendelezo wa ubora waliouonyesha msimu uliopita. Lakini kwa wengine, iwe ni kutokana na majeraha, kuporomoka kwa viwango au kushindwa kufikia matarajio yaliyowekwa juu yao, msimu wa 2026/27 ni fursa ya kurejea katika viwango vyao bora. Twende pamoja!

MAFUN 03

COLE PALMER

Cole Palmer alihitaji sekunde 31 tu katika mechi ya kwanza ya msimu ili kufikisha idadi ya pasi za mabao alizotoa kwa Chelsea katika Ligi Kuu England msimu mzima uliopita. Mpira wake katika dakika ya kwanza dhidi ya Fulham ulimaliziwa kwa ustadi na Joao Pedro na ukawa miongoni mwa matukio kadhaa yaliyoonyesha ubora wa kiufundi ambao ulikosekana sana msimu uliopita, wakati Palmer alipokuwa akisumbuliwa na matatizo ya utimamu wa mwili pamoja na kushuka kwa kiwango.

Mchanganyiko huo wa matatizo ulimfanya akose nafasi katika kikosi cha England cha kocha Thomas Tuchel kilichokwenda Kombe la Dunia 2026.

Baadaye wawili hao walibadilishana majukumu kwa bao la tatu la Chelsea, ambapo Palmer kwa utulivu aliupitisha mpira katikati ya miguu ya kipa Bernd Leno na kufunga bao ambalo hatimaye lilikuwa la ushindi.

Baada ya kupata mapumziko wakati wa kiangazi na kufanya maandalizi bora ya msimu, Palmer anaonekana kuwa tayari kurejesha kiwango alichoonyesha katika misimu yake miwili ya kwanza Chelsea. Katika misimu hiyo, 2023/24 na 2024/25, Palmer alifunga mabao 37 na kutoa pasi 19 za mabao. Ni wachezaji wawili tu, Mohamed Salah (75) na Erling Haaland (57) waliohusika katika mabao mengi zaidi kuliko Palmer aliyehusika katika mabao 56.

Namba 10 huyo wa Chelsea alikuwa kila mahali dhidi ya Fulham mechi iliyopita. Alipiga mashuti matano, idadi kubwa zaidi kwa Chelsea, huku pia akigusa mpira mara tisa ndani ya eneo la hatari la Fulham, zaidi ya mchezaji mwingine yeyote wa Chelsea. Pia alifanya kazi kubwa bila mpira. Alishinda mipambano 10, idadi kubwa zaidi katika mchezo huo na kurejesha umiliki wa mpira mara saba pia zaidi ya mchezaji mwingine yeyote wa Chelsea. Iwapo ataendelea kuwa fiti, ni vigumu kuamini kwamba mchezaji mwenye kipaji kama Palmer anaweza kupitia tena msimu mwingine mbaya.


MAFUN 01

MARTIN ODEGAARD

Martin Odegaard amepitia misimu kadhaa migumu Arsenal, huku nahodha huyo akipambana zaidi na utimamu wa mwili msimu uliopita, ambapo alicheza asilimia 35 tu ya dakika zote zilizokuwepo.

Odegaard amefunga mabao manne pekee katika misimu miwili iliyopita ya Arsenal, na ingawa timu hiyo ilitwaa ubingwa msimu uliopita itakuwa vigumu kusema alikuwa miongoni mwa wachezaji muhimu zaidi katika mafanikio hayo.

Hata hivyo, kiwango chake akiwa na Norway katika Kombe la Dunia 2026 kilitoa dalili nzuri kwamba fundi huyo kichwani alikuwa akianza kurejesha ubora wake wa zamani. Odegaard alikuwa muhimu sana katika ushindi wa Arsenal wa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza wa msimu wa 2026/27.

Kama inavyoonyeshwa na mtandao wa pasi wa Arsenal, pembetatu yao ya upande wa kulia iliyoundwa na Odegaard, Bukayo Saka na Ben White ilirejea katika ubora wake, huku raia huyo wa Norway kwa mara nyingine akiongoza ujenzi wa mashambulizi ya Arsenal kwa kasi na malengo.

Ukiondoa mabeki, ni Declan Rice pekee aliyegusa mpira mara nyingi zaidi na kukamilisha pasi nyingi zaidi kuliko Odegaard. Hata hivyo, ni muhimu kutambua kwamba pasi za Odegaard zilifanyika katika maeneo ya juu zaidi na yenye thamani kubwa zaidi.

Kwa bao lake la kipindi cha pili, tayari amefunga mabao mengi zaidi katika mashindano yote msimu wa 2026/27 ikiwa ni mawili kuliko aliyofunga katika mechi 36 msimu uliopita, ambapo alifunga moja pekee. Pia alifunga katika ushindi wa Ngao ya Jamii dhidi ya Manchester City. Odegaard anaonekana mwenye nguvu mpya, ushawishi mkubwa na ubora kichwani na miguuni.


MAFUN 02

ANTHONY ELANGA

Anthony Elanga hajafikia kiwango kilichotarajiwa tangu alipohamia Newcastle United kutoka Nottingham Forest kwa ada ya Pauni 55 milioni.

Katika msimu wake wa mwisho Forest, Elanga alifunga mabao sita na kutoa pasi 11 za mabao, idadi iliyomfanya kuwa mchezaji wa tatu kwa pasi nyingi za mabao kwenye ligi.

Lakini, msimu wake wa kwanza Newcastle alishindwa kufunga hata bao moja katika mechi 32 za EPL, akianza mechi 14 pekee, jambo linaloashiria kwamba hakuwa amefanya vya kutosha kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza.

Hata hivyo, kitu ambacho hakikuwahi kumpotea Elanga ni kasi yake ya kutisha. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Sweden alifikisha kasi ya juu ya kilomita 34.9 kwa saa katika mchezo wa kwanza wa Newcastle dhidi ya Liverpool, ikiwa ni ya tatu zaidi kuliko mchezaji yeyote katika ligi siku hiyo.

Kasi hiyo ilionekana wazi katika bao lake. Alikimbilia pasi ya kupenyezwa kutoka kwa William Osula, akimwacha Milos Kerkez nyuma, kabla ya kumalizia mpira kwa ustadi na kufunga. Bao hilo lilimaliza mfululizo wa mechi 40 EPL bila kufunga na kuwa la kwanza la ligi akiwa Newcastle, katika mechi ya 33 ya ligi akiwa na klabu hiyo.

Siyo kila timu itakuwa dhaifu dhidi ya mashambulizi ya kushtukiza kama Liverpool ilivyokuwa wakati huu, lakini Newcastle ikiwa na Harvey Barnes na Elanga pembeni mwa Yoane Wissa na Osula wenye uwezo mkubwa wa kiufundi, inaweza kuwa tishio kubwa katika mashambulizi ya kushtukiza. Hapo ndipo Elanga aling'ara akiwa Forest.

Forest ilikuwa na wastani wa umiliki wa mpira wa asilimia 40.8 katika msimu wake wa mwisho klabuni hapo, kiwango kinachofanana na asilimia 39.2 ya umiliki wa mpira ambao Newcastle ilikuwa nao dhidi ya Liverpool. Iwapo mwenendo huo utaendelea, Newcastle inaweza kumpa Elanga mazingira ambayo hapo awali yalimsaidia kuonyesha kiwango chake bora.