Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Real Madrid imeanza mambo yake

MADRID Pict

Muktasari:

  • Mshambuliaji Kylian Mbappe aliibuka shujaa wa mchezo huo baada ya kufunga hat-trick, huku Real Madrid ikipata ushindi wake wa kwanza wa nyumbani katika msimu huu wa LaLiga.

MADRID, HISPANIA: MCHEZO  wa kwanza wa Jose Mourinho kurejea katika Uwanja wa Santiago Bernabeu akiwa kocha wa Real Madrid umeanza kwa ushindi mkubwa baada ya vigogo hao wa Hispania kuichapa Real Sociedad mabao 4-1.

Mshambuliaji Kylian Mbappe aliibuka shujaa wa mchezo huo baada ya kufunga hat-trick, huku Real Madrid ikipata ushindi wake wa kwanza wa nyumbani katika msimu huu wa LaLiga.

Mbappe aliondoka na mpira wa mchezo baada ya kufunga mabao matatu, lakini yeye pamoja na Jude Bellingham ndio waliovuna sifa kubwa kutokana na kiwango walichoonyesha.

Gazeti la michezo la Hispania, Marca, lilimpa Mbappe alama 10/10 kutokana na kiwango chake, huku Bellingham akipewa alama tisa.

MADR 01

Marca ilimtaja Mbappe kuwa ni mchezaji “mharibifu” kutokana na namna alivyoitesa safu ya ulinzi ya Real Sociedad, lakini sifa iliyopewa Bellingham nayo ilikuwa ya kipekee, kwani gazeti hilo lilimtaja kama “usajili bora wa Mourinho.”

Katika kipindi cha kwanza, Marca ilimpa Bellingham alama 8/10 na kueleza:

“Alitoa taswira ya kuwa katika hali bora kabisa ya kimwili, bila kupoteza ile cheche aliyoiibua tena kwenye Kombe la Dunia.

“Alikuwa mwenye nguvu, mkali, akionekana kila sehemu na akicheza kwa uwazi pamoja na usahihi. Alikuwa tishio kubwa pembezoni mwa eneo la hatari na alitengeneza nafasi nzuri kwa Mbappe na Vini [Vinicius Jr].

MADR 02

“Alidai kupigwa faulo ya wazi pembezoni mwa eneo la hatari, lakini mwamuzi Busquets Ferrer hakukubaliana naye. Pia alimsababishia Yangel Herrera kuonyeshwa kadi ya njano.”

Katika kipindi cha pili, Marca ilizidisha sifa zake kwa Bellingham na kumpa alama 9/10, ikiandika:

“Wa kiwango cha juu. Makofi ya mashabiki wa Bernabeu wakati akitolewa yalikuwa uthibitisho wa mchezo wake mzuri uliokuwa umejaa kujituma, juhudi na vipindi vya ubora.

“Alifanya kazi ya kiwango cha juu pamoja na Mbappe pembezoni mwa eneo la hatari, jambo lililomwacha Mfaransa huyo akiwa peke yake na kufunga bao la 2-1. Ulikuwa ufundi wa kiwango cha dunia.

MADR 03

“Lakini bado kulikuwa na zaidi. Juhudi zake binafsi pamoja na moyo wake wa kupambana vilisababisha pasi ya mwisho aliyotoa kwa Vinicius kufunga bao la tatu.

“Bellingham ni usajili bora wa Mourinho.”

Hizo zilikuwa sifa kubwa kwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23.

Mbappe aliipa Real Madrid uongozi dakika ya 40, kabla ya Luka Sucic kusawazisha dakika nne baadaye. Hata hivyo, mshambuliaji huyo wa Ufaransa aliirejeshea Madrid uongozi katika dakika ya 60, kabla ya Vinicius Jr kuongeza bao la tatu dakika ya 68.

Mbappe alikamilisha hat-trick yake dakika 10 kabla ya mchezo kumalizika, akifunga bao la nne na kuipa Real Madrid ushindi mnono wa mabao 4-1.

MADR 04

Ulikuwa pia mwanzo mzuri wa kurejea kwa Mourinho katika Santiago Bernabeu, zaidi ya miaka 13 tangu mchezo wake wa mwisho wa nyumbani akiwa kocha wa Real Madrid.

Real Madrid ilifanikiwa kubadilika baada ya kuonyesha kiwango kisichokuwa na mpangilio mzuri katika kipindi cha kwanza, kabla ya kuingia kipindi cha pili ikiwa na kasi, ukali na ufanisi mkubwa mbele ya lango.

Kabla ya mapumziko, mashabiki wa Madrid waliwazomea wachezaji wao kutokana na mwanzo wa kusuasua, ambapo timu hiyo ilionekana kukosa mwendo, kupoteza mipira kwa uzembe na kuwa katika hatari kila iliposhambuliwa kwa kushtukiza.

“Daima kuna hali ya haki katika kuzomewa na kushangiliwa, na kuzomewa mara moja moja hakumdhuru mtu yeyote  kunakusaidia kukua,” Mourinho amesema katika mkutano na waandishi wa habari.

“Sote tunaujua Santiago Bernabeu na tunajua jinsi mashabiki wake walivyo na mahitaji makubwa. Ninafurahi sana na namna wachezaji wangu walivyoitikia presha na kucheza kipindi cha pili vizuri, ambacho tungeweza hata kufunga mabao zaidi.”

Real Sociedad ndiyo iliyoonekana kuwa tishio kubwa mwanzoni mwa mchezo na ilikaribia kupata bao la kuongoza dakika ya 10.

Kwa Mourinho, ushindi huo umeufanya mchezo wake wa kwanza wa kurejea Bernabeu kuwa wa kuvutia zaidi, huku Mbappe akianza msimu kwa hat-trick na Bellingham akionyesha kwa nini amekuwa sehemu muhimu ya mipango ya kocha huyo.