Pochettino mguu mmoja nje Marekani
Muktasari:
- Mkataba wa Pochettino na Marekani unafikia tamati katika kipindi hiki cha Fainali za Kombe la Dunia na mabosi wa shirikisho la soka nchi hiyo wameonyesha utayari wa kumpa mkataba mpya lakini mwenyewe anaonekana ameshaamua vinginevyo.
LOS ANGELES, MAREKANI: BAADA ya kuiongoza Marekani kufika hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia 2026, Mauricio Pochettino anajiandaa kuachana na timu hiyo na kujiunga na mojawapo ya klabu za Ulaya.
Inaripotiwa kwamba licha ya Shirikisho la Soka Marekani kuonyesha nia ya kuendelea na Kocha huyo raia wa Argentina, Pochettino ameonyesha kuhitaji changamoto mpya jambo linaloilazimisha Marekani kuanza kusaka mkataba wake.
Mkataba wa Pochettino na Marekani unafikia tamati katika kipindi hiki cha Fainali za Kombe la Dunia na mabosi wa shirikisho la soka nchi hiyo wameonyesha utayari wa kumpa mkataba mpya lakini mwenyewe anaonekana ameshaamua vinginevyo.
AC Milan inayoshiriki Ligi Kuu Italia ‘Serie A’ inatajwa kuwa klabu ambayo inawania kwa udi na uvumba saini ya kocha huyo huku pia akiwa na ofa kutoka kwa baadhi ya klabu zinazoshiriki Ligi Kuu England.
Baada ya timu ya taifa ya Marekani kupoteza mechi dhidi ya Ubelgiji, Pochettino alikataa kujibu maswali kuhusu mustakabali wake.
“Huu si wakati wa kuzungumzia jambo hilo.Kwa sasa hakuna muda maalumu uliowekwa wa kufanya uamuzi,” amesema.