Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Harry Kane afunguka kurudi England

HARRY Pict

Muktasari:

  • Kane, ambaye aliwahi kuchezea Tottenham Hotspur, bado ana miaka miwili kwenye mkataba wake wa sasa, lakini Bayern Munich tayari imeonyesha nia ya kumwongezea mkataba wakati huu na anahusishwa na timu kibao.

LONDON, ENGLAND: KAPTENI wa timu ya taifa ya England, Harry Kane, 32, amefuta tetesi za kutaka kurejea tena England na kusisitiza yupo tayari kusaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia.

Kane, ambaye aliwahi kuchezea Tottenham Hotspur, bado ana miaka miwili kwenye mkataba wake wa sasa, lakini Bayern Munich tayari imeonyesha nia ya kumwongezea mkataba wakati huu na anahusishwa na timu kibao.

Katika mkataba wake kuna kifungu maalum kinachomruhusu kuondoka mwisho wa msimu huu kwa dau la Pauni 56.7 milioni na Tottenham ina chaguo la kumsajili tena ikiwa itahitaji kufanya hivyo,

Harr 01

Nyota huyo wa Bayern, ambaye alitwaa taji la Bundesliga msimu uliopita, kwa msimu huu tayari amefunga mabao 19 kwa timu yake hiyo na England.

Akizungumzia tetesi za kuondoka Kane amesema: "Kuhusu kubaki hapa muda mrefu zaidi? Ndiyo, hili lipo na linaweza likatokea kwa asilimia kubwa. Sijazungumza na Bayern kuhusu hilo kwa sasa, lakini kama mazungumzo hayo yataanza, niko tayari kubaki hapa. Kwa sasa tunapitia kipindi kizuri sana, kwa hiyo sifikirii kuondoka, kuhusu kurudi Ligi Kuu England, sijui. Kama ungeliniuliza mara tu baada ya kujiunga na Bayern, ningesema kweli nataka kurudi, lakini sasa nimekaa hapa kwa miaka michache, mawazo hayo yamepungua kichwani mwangu, lakini siwezi kusema sitarudi kabisa."

Harr 02

"Nimejifunza katika soka fursa na nyakati hubadilika, na mambo huja kwa mpangilio wake. Kwa sasa, mimi niko Bayern na nitaipambani kwa nguvu zangu zote."

"Kama kutakuwa na mazungumzo ya kuongeza mkataba, tutaona, lakini bado nina mkataba wa kuwa hapa kwa msimu huu na mwingine mbele. Kwa hiyo hakuna presha wala haraka."