Gavi, Paredes wazua vurugu
Muktasari:
- Hispania ilitwaa ubingwa wake wa pili wa Kombe la Dunia baada ya kuichapa Argentina bao 1-0 katika muda wa nyongeza, na kurejea kileleni kwa mara ya kwanza tangu kizazi cha dhahabu kilichotwaa taji hilo nchini Afrika Kusini mwaka 2010.
NEW YORK, MAREKANI: SHEREHE za Hispania baada ya kutwaa Kombe la Dunia 2026 ziligubikwa na sintofahamu kufuatia mzozo uliotokea mara tu baada ya filimbi ya mwisho, uliowahusisha kiungo wa Barcelona, Gavi, na nyota wa Argentina, Leandro Paredes.
Hispania ilitwaa ubingwa wake wa pili wa Kombe la Dunia baada ya kuichapa Argentina bao 1-0 katika muda wa nyongeza, na kurejea kileleni kwa mara ya kwanza tangu kizazi cha dhahabu kilichotwaa taji hilo nchini Afrika Kusini mwaka 2010.
Hata hivyo, wakati wachezaji wa Hispania wakianza kusherehekea ushindi huo, hali ilichafuka baada ya kuzuka kwa mzozo kati ya Gavi na Paredes.
Picha zilizosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii zilimuonyesha Paredes akiwa na hasira kali akimkabili Gavi, licha ya kiungo huyo wa Barcelona kutocheza hata dakika moja katika fainali hiyo.
Tukio hilo lilivuta hisia za mashabiki wengi, huku likiongeza sura nyingine ya mvutano uliojitokeza baada ya mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa kati ya mataifa hayo mawili.
Ingawa chanzo halisi cha mzozo huo hakikufahamika mara moja, picha na video zilionyesha hali ya taharuki kabla ya wachezaji na maofisa wa timu zote kuingilia kati na kutuliza vurugu.
Badala ya sherehe za ubingwa pekee kuwa gumzo, tukio hilo la Gavi na Paredes nalo lilitawala mijadala baada ya fainali ya Kombe la Dunia 2026.
Paredes apoteza utulivu
Kiini cha vurugu hizo kilikuwa kiungo mkongwe wa Argentina, Leandro Paredes.
Picha zilizosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii zilimuonyesha Paredes akiwa na hasira kali akimkabili kiungo wa Barcelona, Gavi, ambaye hakupata nafasi ya kucheza katika fainali hiyo.
Mbali na Gavi, Paredes pia aliingia kwenye mabishano makali na beki Eric Garcia wakati sherehe za Hispania zikiendelea.
Scaloni aliingilia kati haraka akijaribu kuwatenganisha wachezaji wake kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Licha ya taharuki hiyo, maofisa wa timu zote walifanikiwa kutuliza hali na kuzuia vurugu hizo kuendelea.
Hispania ikaendelea na shamrashamra za kutwaa taji lake la pili la dunia, huku Argentina ikiondoka na majonzi makubwa baada ya kukosa nafasi ya kuandika historia ya kutwaa Kombe la Dunia mara mbili mfululizo.