Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga yatesti mitambo, yampiga mtu wiki

WIKI Pict

Muktasari:

  • Katika mchezo huo mabao ya Yanga yamefungwa na Chadrack Boka akipokea asisti ya Maxi Nzengeli, Albert Kangwanda akitengenezewa na Cheikh Toure.

Yanga imecheza mchezo wa kwanza wa kirafiki dhidi ya Magereza ya Dar es Salaam ikishinda kwa mabao 7-2.

Mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa mazoezi wa timu hiyo wa Avic, Yanga imetumia karibu wachezaji wake wote walioingia kambini kujiandaa na msimu mpya.

Katika mchezo huo mabao ya Yanga yamefungwa na Chadrack Boka akipokea asisti ya Maxi Nzengeli, Albert Kangwanda akitengenezewa na Cheikh Toure.

Mabao mengine yamefungwa na Laurindo Aurelio 'Depu' aliyefunga mara mbili akitumia asisti ya Allan Okello, Edmund John, Okello na Abdulnassir Mohammed 'Casemiro'.

Kocha wa Yanga,  Manqoba Mngqithi ametumia mchezo huo kupima mazoezi ya wachezaji wake yaliyofanyika kwa wiki mbili sasa.

Yanga imekuwa ikifanya mazoezi makali ikitumia saa nne ikiendelea kujipanga na hesabu za msimu mpya.

Inaelezwa kwa ratiba ya Mngqithi kikosi hicho kitakuwa kila baada ya mazoezi ya siku saba kitacheza mchezo wa kirafiki kupima kiwango cha utimamu wa kile walichojifunza wachezaji.