Yanga ikizubaa tu Mukoko Tonombe anasepa
Muktasari:
INASEMEKANA kiwango cha kiungo mkabaji wa Yanga, Mukoko Tonombe kimeikuna miamba ya soka la Afrika Kusini, Kaizer Chiefs.
INASEMEKANA kiwango cha kiungo mkabaji wa Yanga, Mukoko Tonombe kimeikuna miamba ya soka la Afrika Kusini, Kaizer Chiefs.
Za Chinichini imepenyezewa kutoka Sauzi kuwa Kaizer inamfuatilia kwa ukaribu kiungo huyo wa kimataifa wa DR Congo.
Kutokana na uwepo wa uvumi huo, Yanga wanapaswa kuwa makini na mchezaji wao huyo ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi chao vinginevyo inaweza kula kwao.
Yanga inakumbuka ilipigwa bao na Simba kwa Bernard Morrison hivyo kama itazembea tena kwa Mukoko hasa kwenye ishu za kimkataba inaweza kumpoteza mchezaji huyo.