Wanigeria wa Yanga wafundwa
KABLA ya kuwavaa Yanga, Rivers United wamewekwa kitako juzi na kufundwa sheria zote za mpira wa miguu zilizorekebishwa.
Habari zinasema uongozi ulifanya hivyo juzi ukihofia lolote linaweza kutokea kwenye mechi dhidi ya Yanga na kuwababaisha wachezaji wao ambao wengi ni wapya na wageni kimataifa.
Kwenye somo hilo walifundishwa sheria zilizofanyiwa maboresho na Fifa ambazo mara kadhaa huwachanganya wachezaji na walisimamiwa na marefa wawili waliobobeba kwenye Ligi Kuu ya Nigeria katika Uwanja wa Adokiye.