Tanzania, Uganda na Kenya kuandaa Afcon 2027
Rasmi Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limepitisha mataifa ya Tanzania, Kenya na Uganda kuandaa michuano ya Afcon 2027.
Nchi hizo ziliwasilisha ombi walilobatiza jina la Pamoja Bid na itakuwa mara ya kwanza ukanda wa Afrika Mashariki kuandaa michuano hiyo mikubwa ya soka Afrika.
Kamati ya Utendaji CAF imetangaza uamuzi huo nchini Misri leo, pia Morocco imechanguliwa kuandaa Afcon 2025.