Polisi Tanzania, Wembe zawania beki Fufuni
Muktasari:
- Chanzo cha ndani ya timu hiyo kimeliambia Mwanaspoti kuwa, baada ya kumkosa Kocha Suleiman Mohamed ‘Gamera’ sasa hasira zao wamezihamishia kwa aliyekuwa mchezaji wa kikosi hicho, Filex.
POLISI Tanzania kutoka Tanzania Bara na Wembe ya Zanzibar, zinawinda saini ya aliyekuwa beki wa kushoto wa Fufuni, Filex Bryson.
Chanzo cha ndani ya timu hiyo kimeliambia Mwanaspoti kuwa, baada ya kumkosa Kocha Suleiman Mohamed ‘Gamera’ sasa hasira zao wamezihamishia kwa aliyekuwa mchezaji wa kikosi hicho, Filex.
Chanzo hicho kimesema, bado timu hiyo ina nia ya kumchukua mchezaji huyo kabla ya ligi kumalizika hivyo uongozi upo katika mazungumzo.
Akizungumza na Mwanaspoti, Mchezaji huyo amekiri kuwepo kwa mazungumzo na timu hizo ijapokuwa hawajafikia muafaka wowote hadi sasa.
“Nikweli timu hizo zinanihitaji lakini bado hatujafikia muafaka wa mazungumzo na Wembe wanasitasita,” amesema.