Mtanzania kupanda ulingoni Dubai
BONDIA Jesca Mfinanga bondia namba mbili kwa ubora Tanzania katika uzito wa kilo 54 amepima uzito leo tayari kwa kushukaka ulingoni kesho kupigana Avril Mathie ambaye ni bondia namba 43 duniani katika uzito huo Dubai.
Akizungumza na Mwanaspoti Katibu wa Kamisheni ya ngumi za kulipwa Tanzania amesema Jesca Mfinanga atashuka katika pambano lake la 4 tangu aanze kucheza ngumi za kulipwa nchini.
“Jesca aliondoka Septemba 16 kuelekea Dubai na kesho atashuka dimbani kucheza dhidi ya Avril Mathie ambae ni bondia namba 4 kwa ubora nchini Australia na 43 kwa ubora duniani.
IMEANDIKWA NA LILIAN MUKULU