Mtanzania Geay atwaa medali ya fedha Boston Marathon
Muktasari:
- Hiyo ni mara ya pili Geay kushiriki mbio hizo kubwa za pesa, awali ilikuwa msimu uliopita na kumaliza wanne
Mtanzania, Gabriel Geay ametwaa medali ya fedha ya mbio za Boston marathoni ziluzomalizika jioni hii nchini Marekani.
Geay aliachwa kwa sekunde tisa na bingwa mtetezi raia wa Kenya, Evans Chebet aliyetumia saa 2:05:54.
Mtanzania huyo anayeshikilia rekodi ya taifa ya marathoni
ametumia saa 2:06:04 kumaliza mbio hiyo.
Mkenya mwingine Benson Kipruto amehitimisha tatu bora akitumia 2:06:06 huku mwanariadha mwenye kasi zaidi duniani kwenye marathon, Eliud Kipchoge amemaliza wa sita.