Majimaji waingilia mlango wa nyuma
Muktasari:
- Wachezaji hao wameingia kupitia mlango mdogo kinyume na Kanuni za Ligi Kuu zinazowataka kuingia kupitia mlango mkuu.
Wachezaji wa Majimaji FC ya mjini hapa wameingia uwanjani kwa kupitia mlango wa nyuma jambo linaloaminiwa kuwa linahusiana na imani za kishirikina.
Wachezaji hao wameingia kupitia mlango mdogo kinyume na Kanuni za Ligi Kuu zinazowataka kuingia kupitia mlango mkuu.
Mwandishi ameshuhudia basi la Majimaji likiingia Uwanjani tupu huku wachezaji wakiwa tayari wamejifungia vyumbani.
Katika hatua nyingine, nyota wa Yanga wameingia na basi lao kupitia mlango mkuu na kushuka kawaida kwenda vyumbani.