Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Lukuvi aenziwa Mkutano Mkuu wa Yanga 

LUKUVI Pict

Muktasari:

  • Lukuvi aliyekuwa Mbunge wa Isimani, Mkoa wa Iringa, kuanzia mwaka 1995, akihudumu kwa miaka 30, alifariki dunia Machi 25, 2026, kwa mshtuko wa Moyo, wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

ALIYEKUWA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), William Lukuvi, ameenziwa katika Mkutano Mkuu wa Yanga, unaofanyika leo Jumapili ya Agosti 2, 2026, kwenye Ukumbi wa The Super Dome, Masaki, jijini Dar es Salaam.

Lukuvi aliyekuwa Mbunge wa Isimani, Mkoa wa Iringa, kuanzia mwaka 1995, akihudumu kwa miaka 30, alifariki dunia Machi 25, 2026, kwa mshtuko wa Moyo, wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Katika mkutano wa leo, mbali na Lukuvi, wanachama wengine wa Yanga walioenziwa ni Yusuph Mwandami, Stephen Hyera, Samson Mwakalinga, Damian Kinyunyu, Kulwa Mussa, Rajabu Selemani, Musa Monde, Eddah Mkama, Andrew Msolo, Kanyika Mshana, Beatus Linda, Adventina Mwanamaya, Saidina Amani, John Makotta, Alex Msamba, Ramadhani Ramadhani, Ruya Fumbogoro na Athumani Puga.

Yanga inafanya mkutano wake mkuu leo Jumapili ya Agosti 2, 2026, kwenye Ukumbi wa The Super Dome, ukiwa na ajenda 14, huku miongoni mwa hizo ni Uchaguzi Mkuu wa kuwachagua, Rais, Makamu wa Rais na wajumbe watano watakaounda Kamati ya Utendaji kwa miaka minne ijayo kuanzia sasa.