Iman Makongo Mwandishi Bora wa Michezo Tanzania
Muktasari:
Imani ameshinda Tuzo hiyo kupitia habari yake ya maisha ya wanariadha wa mikoa ya Singida na Manyara .
Mwandishi wa Habari wa Mwanaspoti, Iman Makongoro ameshinda Tuzo ya Habari za Michezo Sanaa na Utamaduni kwa mwaka 2017.
Imani ameshinda Tuzo hiyo kupitia habari yake ya maisha ya wanariadha wa mikoa ya Singida na Manyara .
Mwandishi huyo ameandika namna ambavyo wanatoka kwenye mazingira magumu ya maisha lakini wameweza kuwa mastaa nchini na duniani kwa ujumla.
Baadhi ya wanariadha hao ni Samson Ramdhani na Alphonce Felix Simbu.
Gazeti la Mwanaspoti ni la michezo na miongozi mwa magazeti yanayochapishwa katika Kampuni ya Mwananchi Communications LTD ambayo pia inazalisha magazeti mengine ya Mwananchi na The Citizens.