Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

CAF yatoa mkeka kwa Yanga, Simba

CAF Pict

Muktasari:

  • Katika mashindano hayo Tanzania itawakilishwa na Yanga na Simba katika Ligi ya Mabingwa huku Azam na Singida Black Stars zitawakilisha katika Kombe la Shirikisho.

CAIRO, MISRI: SHIRIKISHO la Soka Afrika(CAF) imetangaza rasmi kalenda ya mechi za msimu wa 2026/27 wa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika.

Katika mashindano hayo Tanzania itawakilishwa na Yanga na Simba katika Ligi ya Mabingwa huku Azam na Singida Black Stars zitawakilisha katika Kombe la Shirikisho.

Msimu uliopita klabu za Tanzania ziliweka rekodi kwa zote kuvuka kucheza hatua ya makundi ya mashindano hayo, lakini zilishindwa kufuzu kwa hatua robo fainali.

Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, msimu wa 2026/27 utaanza kwa hatua ya kwanza ya mchujo, ambapo mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa kati ya 4-6 Septemba 2026, huku marudiano yakifanyika 11-13 Septemba 2026.

Hatua ya pili ya mchujo itaanza kwa mechi za mkondo wa kwanza kati ya 16-18 Oktoba 2026, kabla ya marudiano kuchezwa 23-25 Oktoba 2026.

Baada ya hatua za mchujo kukamilika, hatua ya makundi ya mashindano yote mawili itaanza mwishoni mwa mwezi Novemba 2026.


Ratiba ya hatua za mchujo

Hatua ya kwanza (Mkondo wa kwanza): 4–6 Septemba 2026

Hatua ya kwanza (Marudiano): 11–13 Septemba 2026

Hatua ya pili (Mkondo wa kwanza): 16–18 Oktoba 2026

Hatua ya pili (Marudiano): 23–25 Oktoba 2026

Ratiba ya hatua ya makundi

Mzunguko wa 1: 27–29 Novemba 2026

Mzunguko wa 2: 4–6 Desemba 2026

Mzunguko wa 3: 18–20 Desemba 2026

Mzunguko wa 4: 8–10 Januari 2027

Mzunguko wa 5: 15–17 Januari 2027

Mzunguko wa 6: 22–24 Januari 2027

Ratiba ya hatua za mtoano

Robo fainali (Mkondo wa kwanza): 26–28 Februari 2027

Robo fainali (Marudiano): 5–7 Machi 2027

Nusu fainali (Mkondo wa kwanza): 9–11 Aprili 2027

Nusu fainali (Marudiano): 16–18 Aprili 2027

Fainali: Itachezwa kati ya 9 Mei na 31 Mei 2027, kulingana na ratiba itakayothibitishwa na CAF baadaye.