Azam: Poleni Simba
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC wametuma salamu za pole kwa uongozi wa Simba kufuatia kifo cha Zakaria Hans Poppe.
Hans Poppe alifariki Dunia jana usiku Septemba 10 katika hospitali ya Aga Khan amegusa watu wengi wa soka na kutoa pole zao ikiwemo taasisi na mashabiki mbalimbali.
Azam wameandika salamu zao za pole katika mtandao wao wa Instagram.
"Poleni sana uongozi na mashabiki wa timu ya Simba kwa kuondokewa na mpendwa wenu, Zakaria Hans Poppe,"