Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Dili iliyokufa - 43

HADITHI - 43 Pict

ILIPOISHIA

Hapo ndipo nilipokumbuka. Wakati ule nilipokuwa nakwenda  kwake kufuatia  dawa ya  mume wangu akanichukua  hadi mahali hapo ambapo alikwenda  kuniingiliakimwili akajidaiananifanyia dawa, kumbe  alikuwa  akinizuga mimi. Na kutoka siku ile sikutamani  tenakurudi kwa mume wangu.

Sasa  kilichomshinda mganga huyokukieleza wazi ni kuniambiakwamba mahali hapo ni pale tulipokwenda akaniingiliakimwili.

“Nimeshapakumbuka”nikamwambia.

SASA ENDELEA...

 

“Basi ndio hapo hapo.Pale ndio mzimuni kwangu. Mambo  yangu yote ya kiganga nayachukua  pale”

Nilitaka nikatae kwenda kwa sababu nilivyowasikia  wakisema na mke wake ni kuwa ameambiwa na majini wake kuwa siku yangu ni leo kisha akasema kafara la majini hao hufanyika usiku na akaongeza zaidi kwa kusema kuwa kama  nitakwenda na mganga huyo peke  yetu ninawezakushituka.

Hapo nikapata tafsiri kuwa huenda ninakwenda kutolewa kafara mimi!

Nikaona  kukataa ile safari kunaweza kuniletea matatizo mengine. Yule mganga anaweza kuhisi  nimewashitukia na hivyo wanaweza kunifanya  lolote baya kabla  ya polisi  kutokea.

Nikamwambia yule mganga.

“Sawa”

“Lakini si kwa sasa, tutasubiri jualitakapokuchwa ndio tuondoke. Wewe na huyo mke mwenzako ndio mtatangulia kwenda”

“Sawa. Hakuna shida”

“Sasa nenda ukabadili  nguo upumzike kidogo kwa  vile  unatoka mjini”

“Sawa”

Nikainuka na kutoka mle chumbani. Niliingia katika kile chumba nilichokuwa ninalala nikabadili nguo kumridhisha mganga huyo ili asijue kama sikuwa mwenzake tena. Sikutaka kumuonesha dalili yoyote ya mabadiliko ambayo  yangemtia  wasiwasi.

Nikiwa mle chumbani baada ya kubadili  nguo  nilimtumia meseji mume wangu  nikamjulisha kuhusu ile safari ya kwenda mzimuni. Akaniambia na yeye atawajulisha polisi.

Baadaye akanitumia meseji na kuniuliza kama ingekuwa vyema polisi wawasili kwa  muda ule kabla hatujaondoka kwenda huko mzimuni.. Niakamjibu “Ndiyo”

Baadaye tena mume wangu akanitumia meseji kunijulisha kwamba wako njiani wanakuja na polisi.

Yule mganga alikuwa mtu wa kushituka shituka. Mara akanifuata mle  chumbani akaniambia.

“Mke wangu naona muda umewadia.  Mnaweza kutangulia  kwenda sasa”

Kwanza niliguna nikamtazama yule mganga kwa  jicho  kali. Nilivyoona atanigundua kuwa  nilikuwa  na kitu nikainamisha uso  wangu chini.

“Sawa, Ngoja  nijiandae” nikamwambia kwa  sauti ya chini.

Mganga huyo alipoondoka kwenye mlango  nikamatumia meseji mume wangu  kumjulisha  kuwa  tunaondoka kwenda  huko mzimuni ambako nilikuwa sijajua tunafuata nini.

Mume wangu alinitumia  meseji kutaka kujua huko mzimuni tulikokuwa  tunakwenda ni wapi lakini sikuweza kumjibu kwani muda ule ule mke mkubwa wa yule  mganga akaingia mle chumbani.

“Umeshajitayarisha?” akaniuliza.

“Tusubiri kidogo” nikamwambia.

“Tusubiri nini?”

Sikuwa na jibu la maana, nikajikuta nikimwambia.

“Nataka niende nikajisaidie”

Nilimaanisha kwenda haja.

“Haya nenda. Unajua  muda nao unakwenda”

Nikatoka  na kuelekea maliwatoni. Lengo langu lilikuwa kuvuta muda ili  hao polisi  wanaokuja watukute pale pale. Nikaingia maliwatoni na kumtumia  meseji mume  wangu kumwambia waharakishe.

Nilipoona  muda unazidi kwenda nikatoka maliwatoni. Mwanamke alikuwa akinisubiri uani. Nikaingia chumbani. Sikuwa na kitu chochote kilichonipeleka humo zaidi ya kupoteza muda. Nikamuoona  na  yeye anaingia. Nikajidai kuweka vitu vyangu sawa kisha tukatoka.

Tukaanza safari ya kwenda huko mzimuni. Nilikuwa  nimechukia kuliko maelezo. Nilikuwa nikizisikia meseji zikiingia kwenye simu yangu nikajua zinatoka  kwa mume wangu lakini sikuweza kuzisoma wala  kuzijibu mbele ya yule mwanamke.

Kila nilipopiga hatua chache nilikuwa natazama nyuma kuwaangalia wale polisi lakini sikuwaona. Tulitembea mwendo mrefu mpaka  tukapotea katika lile  eneo. lakini njia nilikuwa naifahamu na ningeweza kumuelekeza mume wangu endapo ningepata nafasi ya kutumia simu.

Nilikuwa siwezi kupiga wala kutuma meseji kwa sababu ya yule mwanamke niliyekuwa nimefuatana naye. Hivyo nikaona niendeleea kwenda ila mara kwa mara nilikuwa natazama nyuma.

Yule mwanamke naye akawa anatazama nyuma baada ya kuniona mimi nikifanya hivyo mara kwa mara.

Niliporudia tena kwa mara nyingine aliniuliza.

“Unatazama nini?”

“Natazama nyuma kwa sababu za kiusalama. Nataka nihakikishe kuwa tuko salama”

“Mbona huku kwetu ni salama. Hakuna matatizo ya wahuni wala wakabaji kama sehemu zingine”

“Kwenye sehemu sehemu za vichakavichaka  kama hizi, unaweza kuona  watu wanakufuata lakini si watu wazuri”

“Ni  kweli lakini huku kwetu sijaona matukio ya aina hiyo.  Kuna siku ninatumwa peke yangu na ninakwenda  na kurudi bila  matatizo”

“Pengine ni wasiwasi wangu tu. Nahisi labda kuna watu wanatufuata ndiyo  maana natazama  nyuma kila wakati”

“Usiwe na wasiwasi, tupo salama”

Tukaenda huku tukizungumza mpaka  tukafika katika hilo eneo ambalo siku ya kwanza kufika ilikuwa ni siku ile  niliyokuja  na mganga, tukaingia katika huo mzimu wake akanifanyia mambo ya ajabu kisha tukaondoka.

Mbali ya huo mzimu ambao ulizungukwa na mibuyu  mitatu, kulikuwa na  nyumba moja pembeni. Ilikuwa  nyumba iliyojengwa  kwa miti na udongo. Tukaenda katika nyumba hiyo.

Yule  mwanamke akafungua mlango akaingia ndani.

“Karibu, pita ndani” akaniambia.

Nikatazama  nyuma kisha nikaingia. Ndani kulikuwa kiza. Akaenda kufungua  mlango wa kutokea uani na kuuacha wazi. Sasa kidogo  kukawa na mwanga.

“Hii ndiyo  nyumba yetu. Wenyewe tukija tunafikizia  humu” akaniambia yule  mwanamke halafu akafungua mlango wa chumba kimoja wapo.

Akaingia ndani. Baada ya muda kidogo akatoa kichwa na kuniambia.

“Ingia”

Nikaingia. Alikuwa amewasha taa ya kibatari ili kuleta mwanga kwani chumba hicho hakikuwa na dirisha na kilikuwa kimejaa makorokoro.

Kulikuwa na kiti kimoja cha marimba, akaniambia.

“Kaa hapo kwenye kiti”

Nikakaa. Wakati nakaa akaniambia  tena.

“Subiri hapo hapo”

Aliuponiambia hivyo akatoka  mle chumbani. Na mimi nilitaka atoke ili nipate nafasi ya kutumia simu yangu.

Nikatoa simu yangu  na kuishika mkononi. Nikajaribu kupiga namba ya mume wangu lakini niligundua mahali nilipokuwa ama hapakuwa na mtandao au kulikuwa na matatizo ya mtandao. Simu haikwenda. Nikagwaya.

Wakati nazungusha macho yangu huku na huku kukitazama kile chumba huku nikiwazia hatima yangu nilisikia harufu kama ya mafukisho ya mashetani kisha nikasikia sauti ya yule mke wa mganga ikinong’ona kutokachumba cha pili.

“Enyi wafalme wa kiti hiki  ninawaomba mje mule mhanga wenu, muda umeshafika. Mje mmoja mmoja. Utaanza wewe baba wa majini na mke wako kisha watafuatia na hao masubiani ambao ni wasaidiziwako…”

Yale maneno yalinishitua. Nikajiuliza ni viumbe gani wanaoitwa waje wale mhanga wao  na mhanga huo ni upi?

Ghafla nikasikia sauti nyingine ambayo ilikuwa  ni sauti ya yule mganga lakini ilikuwa inakoroma.

“Ndiyo nimekuja…mimi mfalme wa majini…nataka nianze kula mhanga wangu…hauwezi tena kuendelea kuishi katika nyumba yangu…muda wake wa kutolewa kafara umeshafika…”

Sasa  moyo ulikuwa ukinienda mbio huku nikijiuliza ni nani anayeambwa maneno hayo wakati  mimi sikuwa katika chumba hicho.

Nikaona nisimame ili nitoke kule chumbani. Nikasimama haraka na kupiga hatua kuelekea kwenye mlango. Ghafla nikamuona mtu aliyevaa joho lenye rangi tatu nyeupe, nyeusi na nyekundu akiingia mle chumbani.

Ingawa nilimtambua kuwa alikuwa ni yule mganga lakini hakuwa katika sura yake kamili. Alikuwa ameacha kinywa wazi. Meno yake ya mbele yalikuwa yamerefuka na yalikuwa yanatoka damu. Macho yalikuwa yamemtoka.

Ule weusi wa  macho haukuwepo. Macho yake yalikuwa ni meupe tu. Kwa  maneno mengine hayakuwa na mboni.

Alikuwa ameinua mikono yake kama vile alikuwa anataka kuvamia kitu. Vidole vilkuwa vimekaza na kucha zilikuwa ndefu kuliko za kawaida. Hali ya yule mganga ilinishitua zaidi.

Nikawa ninarudi nyuma kumkwepa huku  nikimtazama kwa mshangao.

Wakati narudi nyuma, yeye alikuwa akinifuata kwa taratibu mikono akiwa ameiinua vile vile kama aliyetaka  kunivamia. Ile sauti ya kukoroma ilikuwa ikisikika kutoka midomoni mwake.

“Siku zako za kuishi zinaisha leo. Mimi  ni Kashkash,jini mnywa damu za watu kila mwaka mara tatu…mimi  ndiye niliyekuchagua uolewe na kiti wangu ili muda ukifika ninywe damu yako. Sasa muda huo umeshafika, tulia nilekaramu yangu…!”

Mikono yake ikanivamia ghafla. Nilipiga ukulele mmoja tu kisha sauti yangu ikapotea. Niliendelea kupiga kelele lakini sauti ilikuwa haisikiki. Nilikuwa kama ninayepiga kelele kimoyomoyo au kwenye ndoto.