Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Z. Anto, Sholo Mwamba kusindikiza Miss na Mr Kiziwi kesho

Msanii Ally Mohamed maarufu kwa jina la Z. Anto, msanii wa kughani mashairi Mrisho Mpoto na wa singeli, Sholo Mwamba kesho wanatarajiwa kuburudisha katika fainali za kumsaka Miss na Mr Viziwi kesho.
Fainali hizo zinatarajiwa kufanyika kesho katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini humo.

Akizungumza leo Ijumaa, Oktoba 28,2022 Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa Utamaduni na Michezo, Dk Hassan Abbasi,alisema Z. Anto atawasilisha ujumbe wa changamoto wanazopata viziwi kupitia wimbo wake 'Binti Kiziwi' ambao ni moja ya nyimbo zake zilizoanya vizuri.
Ukiachilia mbali Z. Anto aliwataja Mpoto ,msanii Sholo Mwamba na kuwahakikisha washiriki hawatajutia kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano hayo kwa namna serikali ilivyojipanga kuwapa raha.
Akizungumzia kuhusu mashindano hayo, Dk Abbasi alisema yameiheshimisha Tanzania kwa kuwa wakati yakiwa yameanza kufanyika miaka 12 iliyopita Tanzania inakuwa nchi ya kwanza Afrika kuwa mwenyeji wake.
"Tanzania imefarijika  sana kuwa wenyeji  mashindano haya,kwani pamoja na mambo mengine linasaidia kuwaonyesha viziwi kuwa wanaweza kufanya kila kitu.
Akielezea namna watu watakavyoweza kushiriki Katibu huyo alisema wametoa mialiko kwa watu 1400 kati yao wakiwemo viongozi wakubwa na watu maarufu.

Hata hivyo alisema awali mgeni rasmi alitarajiwa awe Rais samia Suluhu Hassan lakini kutokana na kubanwa na majukumu atawakilishwa na Waziri  wa Jinsia, Wanawake  na makundi maaulum, Dk Doroth Gwajima na Waziri wa sanaa Utamaduni na Michezo, Mohamed Mchengerwa.
Pamoja na kuwepo kwa zawadi nyingine, Dk Abbasi amesema wametoa ofa ya washindi katika vipengele mbalimbali kwenda kutembelea mbuga ya Ngorongoro.
Kwa upande wake Rais wa Chama cha Viziwi Afrika, Habibu Mrope alisema dunia nzima kufika Tanzania sio jambo dogo na kuishukuru namna ambavyo  imewapa ushirikiano katika kipindi  kipindi chote cha maandalizi


Naye Rais wa madhindano ya viziei dunia, Bonita Annlee,amesema mashindano hayo yamesadia kuwaweka viziwi pamoja na kuonyesha dunia kuwa nao wana vipaji kama walivyo watu wa kawaida.