Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

SPURS: Wamebadili mambo mengi kwa haraka sana?

SPURS Pict

Muktasari:

  • Na sasa, kwa kuzingatia kwamba wameshindwa kufunga bao hata moja katika Ligi Kuu England na tayari wametolewa katika moja kati ya mashindano mawili ya vikombe, ni rahisi kufikia hitimisho kwamba jibu la swali hilo hapo juu huenda likawa ‘ndiyo’.

LONDON, ENGLAND: BAADA ya kufanya mabadiliko makubwa katika kikosi, Tottenham Hotspur wameanza vibaya sana msimu wa 2026-27.

Wasiwasi unaongezeka kwamba wachezaji wapya hawataweza kuzoeana haraka vya kutosha na tayari ilionekana kuwa kuna uwezekano wakapata wakati mgumu kukabiliana na mabadiliko makubwa waliyoyafanya katika kipindi cha majira ya joto.

Na sasa, kwa kuzingatia kwamba wameshindwa kufunga bao hata moja katika Ligi Kuu England na tayari wametolewa katika moja kati ya mashindano mawili ya vikombe, ni rahisi kufikia hitimisho kwamba jibu la swali hilo hapo juu huenda likawa ‘ndiyo’.

Kwa mara ya kwanza katika historia yao, katika daraja lolote, Spurs wameanza msimu wakiwa na mechi nne mfululizo bila kufunga bao na, jambo linalotia wasiwasi, hadi sasa hakuna ushahidi mkubwa wa kutosha unaoweza kutegemewa kuonyesha kwamba mambo yatabadilika hivi karibuni kuwa bora.

Uchezaji wao katika kipigo cha Carabao Cup dhidi ya Liverpool cha mabao 3-1 usiku wa Jumanne bila shaka ulikuwa bora zaidi msimu huu. Spurs walitengeneza nafasi mbili kubwa katika kipindi cha kwanza ambazo Lucas Bergvall na Mohammed Kudus walishindwa kuzitumia, na kwa mtazamo mpana walistahili kupata kitu kutoka katika mchezo huo, baada ya kutawala umiliki wa mpira na kutengeneza nafasi bora zaidi.

SPU 01

Lakini, mwishowe, ulikuwa ni mchezo mwingine wa kupoteza. Na kwa sehemu kubwa, kulikuwa na vitu katika uchezaji wao wa kushambulia, huku wakipoteza umiliki wa mpira mapema mno mara kwa mara, na ingawa walifunga bao, lilitokana na mpira wa kutenga. Zaidi ya hayo, walikuwa wakicheza dhidi ya Liverpool iliyosukwa kwa kiasi kikubwa na vijana na wachezaji wa akiba.

Wakati huohuo, upande wa pili wa uwanja, Spurs walikuwa rahisi mno kupenya, na pia walipoteza mpira mara nyingi karibu na lango lao wenyewe. Hawakufanya iwe vigumu vya kutosha kwa Liverpool, na katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza, huenda wangeadhibiwa mara nyingi zaidi na kwa ukali zaidi.

Bila shaka kulikuwa na mambo ya kutia moyo. Baadhi ya mipango ya mashambulizi waliyoitengeza iliipenya Liverpool kwa kuvutia, na mara kadhaa walishindwa kubadilisha nafasi nzuri walizopata kuwa za kufunga, licha ya kuwa na mashuti yenye thamani ya 2.33 yaliyotarajiwa.

Cha kushangaza, hiyo ilikuwa mabao yanayotarajiwa (xG) zaidi dhidi ya timu ya England tangu Desemba 2024, walipocheza dhidi ya Southampton. Lakini ukweli kwamba hawakutumia vizuri zaidi nafasi walizofika na eneo walilolitawala unaongeza zaidi hisia zilizojitokeza tangu mwanzo wa msimu huu kwamba wachezaji hao hawajazoea kabisa kucheza pamoja.

SPU 02

Na hilo linaeleweka. Spurs walitumia zaidi ya Pauni 300 milioni kununua wachezaji wapya katika kipindi cha majira ya joto, na pia walisajili mastaa kadhaa kwa uhamisho huru. Haikutarajiwa kamwe kwamba wangeanza kuelewana mara moja, na kocha Roberto De Zerbi ameeleza hilo pia kupitia vyombo vya habari. “Bado sisi siyo timu,” alisema raia huyo wa Italia baada ya kipigo cha siku ya kwanza dhidi ya Brentford. Spurs wamefanya mabadiliko mengi zaidi katika kikosi cha kwanza kutoka mchezo mmoja hadi mwingine (12) kuliko walivyowahi kufanya katika mechi nne za mwanzo za msimu wowote wa Ligi Kuu England. Huenda siku zote haikuwa uhalisia kubadilisha mambo kwa kiwango hiki kwa muda mfupi na kutarajia matokeo.


NAMBA VIPI?

Kabla ya mchezo dhidi ya Liverpool, walikuwa wamecheza vibaya sana katika mechi nne za kwanza za Ligi Kuu England, wakitengeneza nafasi zenye thamani 2.22 pekee katika mchezo wa wazi, ambazo ni idadi ndogo zaidi kuliko timu nyingine yoyote kwenye ligi.

Na kutokana na uwekezaji mkubwa katika kuwasajili wachezaji wanaoweza kucheza soka analolitaka De Zerbi, pamoja na hamu ya kocha huyo kuwaondoa wachezaji ambao hawakutaka kubaki kama vile Cristian Romero, wamepoteza kwa kiasi kikubwa tishio lao katika mipira ya kutenga, jambo ambalo huenda lilikuwa moja ya mambo machache chanya katika msimu wa 2025-26, ambapo walivunja rekodi ya awali ya Ligi Kuu England mabao yaliyofungwa kutokana na mipira ya kona (18, ingawa wapinzani wao Arsenal walifunga 19).

SPU 03

Katika mechi za ligi msimu huu, Spurs wamekuwa tishio dogo sana kupitia mipira ya kutenga, wakitengeneza nafasi zenye thamani ya 1.22 ambazo ni za saba kutoka mwisho kwa ubora kwenye ligi, huku wakiwa hawajafunga bao. Spurs, bila shaka, bado ni changa kwa maana ya muda ambao imekuwa pamoja, na kulikuwa na dalili huko Anfield kwamba inaweza kuboresha kwa kiasi kikubwa kabla ya muda mrefu.

Pia kuna hoja yenye nguvu kwamba walilazimika kumuunga mkono De Zerbi katika soko la usajili na kufanya mabadiliko mengi katika msimu mmoja wa majira ya joto baada ya kumaliza katika nafasi ya 17 mara mbili mfululizo.

Lakini historia inaonyesha kwamba mabadiliko makubwa kiasi hiki mara chache huleta maboresho ya haraka na makubwa, ambapo Spurs ni timu ya 12 katika ligi hiyo kuwatumia wachezaji wapya walioanza zaidi ya mara 20 katika mechi nne za mwanzo za msimu, ambao hawakucheza hata mchezo mmoja kwa timu hiyo msimu uliotangulia.

SPU 04

Kati ya timu 11 zilizotangulia, ni tano pekee zilizoboresha nafasi katika ligi kutoka msimu mmoja hadi mwingine. Kati ya timu sita ambazo nafasi zao zilishuka, ni moja pekee iliyoshuka daraja, lakini nyingine nne zilimaliza katika nafasi ya 17, juu kidogo tu ya eneo la kushuka daraja.

Na kati ya timu tano zilizoboresha nafasi katika ligi, ni chache zilizoendelea kukua kwa muda mrefu; Spurs 2004-05 na Manchester City 2008-09. Maboresho ya City kwa kiasi kikubwa yalitokana na kuendelea kutumia fedha nyingi mwanzoni mwa enzi ya Sheikh Mansour.

Wakati huohuo, West Ham waliboresha msimamo 2018-19 baada ya kuwasajili wachezaji wengi wapya, lakini walikaribia kushuka daraja msimu uliofuata na sasa wapo Championship. Sunderland walishuka hadi League One baada ya kutumia fedha nyingi katika usajili msimu wa joto kabla ya 2013-14. Chelsea walishuka katika msimamo na kumaliza nafasi ya 10 misimu miwili tu baada ya kufanya mabadiliko makubwa ya wachezaji kabla ya msimu wa 2023-24.

SPU 05

BADO SANA

Hisia kuhusu Spurs ni kwamba mambo hayawezi kuwa mabaya zaidi kuliko msimu uliopita; kwamba kuna ubora mkubwa katika kikosi chao kiasi kwamba hakuna uwezekano wa wao kupambana tena kuendelea kubaki Ligi Kuu. Huenda hilo likawa kweli, lakini hata wachezaji wazuri wanahitaji muda wa kuzoeana, hasa pale ambapo wachezaji wengi kiasi hiki wanaunganishwa kwa wakati mmoja.

Pia kuna jambo lisilo rahisi kupimika, kwamba kuna presha kubwa kwa wachezaji wapya kufanya tofauti ya haraka na kubwa, hasa wale waliosajiliwa kwa fedha nyingi. Savio na Mateus Fernandes wote wana umri wa miaka 22, lakini Spurs wanahitaji wafanye mabadiliko makubwa katika timu. Kuna uwezekano mkubwa kwamba wanaweza kupata wakati mgumu kukabiliana na aina hiyo ya presha. Sandro Tonali, mwenye miaka 26, na Omar Marmoush, 27, wana uzoefu zaidi, lakini bado ni matarajio makubwa kutarajia mengi kutoka kwa yeyote kati yao.

Huenda pia kukawa na uvumilivu mdogo kutoka kwa mashabiki siyo kwa sababu tu ya fedha zilizotumika kuwasajili wachezaji hao, bali kwa sababu hawajapata muda wa kutosha wa kuwazoea na kuwapenda. Kuna mambo machache yanayowaunganisha mashabiki na wachezaji lakini hakuna historia ya pamoja, na hilo litaongeza zaidi presha kwa wachezaji kufanya vizuri mapema badala ya kusubiriwa muda mrefu.

Kwa ujumla, haionekani kama kuna mchanganyiko unaoweza kuleta mafanikio ya haraka, na ushahidi wa awali kutoka katika mwanzo wa msimu wa Tottenham Hotspur unaonyesha kwamba huenda wakapata wakati mgumu.

Spurs walifunga bao huko Anfield, lakini katika ligi, sasa zimepita dakika 407 tangu walipofunga bao lao la mwisho; bao la Joao Palhinha lililokuwa la ‘kubahatisha’ dhidi ya Everton mwishoni mwa msimu uliopita, ambalo liliwasaidia Spurs kubaki katika Ligi Kuu England.