R Kelly ahukumiwa miaka 30 jela
Muktasari:
- Mwimbaji wa Marekani, Robert Kelly maarufu R Kelly leo amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kutumia hadhi yake ya kuwa nyota kuendesha mpango wa kuwadhulumu kingono wanawake na watoto kwa zaidi ya miongo miwili.
Mwimbaji wa Marekani, Robert Kelly maarufu R Kelly leo amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kutumia hadhi yake ya kuwa nyota kuendesha mpango wa kuwadhulumu kingono wanawake na watoto kwa zaidi ya miongo miwili.
Hata hivyo, mawakili wanaomuwakilisha Kelly mwenye umri wa miaka 55, wamesema atakata rufaa kupinga hukumu hiyo.
Hukumu hiyo imetolewa leo ikiwa imepita zaidi ya miaka miwili akiwa rumande katika jela mjini Brooklyn