Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kidjo mwanamuziki wa kwanza Afrika kupata nyota Hollywood Walk of Fame

Muktasari:

  • Mshindi huyo wa Tuzo tano za Grammy alitunukiwa heshima hiyo Jumanne, Agosti 18, 2026, katika hafla iliyofanyika Los Angeles, ambapo alizindua nyota ya 2,854 kwenye barabara maarufu ya Hollywood Boulevard.

Mwanamuziki mashuhuri kutoka Benin, Angélique Kidjo, ameandika historia baada ya kutunukiwa nyota kwenye Hollywood Walk of Fame, na kuwa mwanamuziki wa kwanza Mwafrika na msanii wa kwanza Mweusi kutoka Afrika kupata heshima hiyo kubwa.

Mshindi huyo wa Tuzo tano za Grammy alitunukiwa heshima hiyo Jumanne, Agosti 18, 2026, katika hafla iliyofanyika Los Angeles, ambapo alizindua nyota ya 2,854 kwenye barabara maarufu ya Hollywood Boulevard.

Kidjo, ambaye amekuwa kwenye tasnia ya muziki kwa zaidi ya miongo minne, alitambuliwa katika kategoria ya Recording kutokana na ubunifu wake mkubwa wa kisanii na ushawishi wake duniani.

Muziki wake umesaidia kuunganisha sauti na tamaduni za Afrika Magharibi na hadhira mbalimbali duniani, huku pia akijikita katika shughuli za utetezi wa haki na misaada ya kibinadamu.

Katika hotuba yake ya kupokea heshima hiyo, Kidjo alisisitiza umuhimu mpana wa tukio hilo, akisema utambuzi huo haukumhusu yeye pekee, bali pia Afrika na mchango wake katika muziki na utamaduni wa dunia.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na mwigizaji wa Hollywood Willem Dafoe pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Recording Academy, Harvey Mason Jr, ambao walimsifu Kidjo kwa mafanikio yake ya kisanii na athari zake nje ya muziki.

Aidha, Agosti 18 ilitangazwa rasmi kuwa Siku ya Angélique Kidjo mjini Hollywood.