Mahrez aipeleka Algeria mtoano
Muktasari:
- Mabingwa hao wa Afcon 2019 ameondoa gundu la kukomea hatua ya makundi kwenye Afcon mbili zilizopita, shukrani kwa bao hilo la kipindi cha kwanza lililofungwa na Mahrez baada ya adhabu ya penalti kufuatia makosa ya Ismahila Ouedraogo.
RABAT, MOROCCO: WINGA wa boli, Riyad Mahrez alifunga bao lake la tatu katika mechi mbili alizocheza kwenye mashindano ya Afcon 2025, akitikisa nyavu kwa mkwaju wa penalti kuipa Algeria ushindi wa 1-0 dhidi ya Burkina Faso mjini Rabat na hivyo kutinga hatua 16 bora.
Mabingwa hao wa Afcon 2019 ameondoa gundu la kukomea hatua ya makundi kwenye Afcon mbili zilizopita, shukrani kwa bao hilo la kipindi cha kwanza lililofungwa na Mahrez baada ya adhabu ya penalti kufuatia makosa ya Ismahila Ouedraogo.
Winga huyo wa zamani wa Manchester City, Mahrez, ambaye alifunga mara mbili katika mechi ya kwanza ambayo Algeria iishinda 3-0 dhidi ya Sudan, alifunga mkwaju wa penalti kwenye kona ya goli na kumtesa kipa Herve Koffi.
Burkina Faso ilionekana kujibu vyema mashambulizi na nusura mbili isiwazishe bao kupitia kwa Pierre Kabore dakika chache kabla ya mapumziko.
Burkina Faso iliendelea kushambulia kwenye kipindi cha pili bila ya mafanikio, huku kipa wao Koffi, naye akilazimika kuokoa hatari kadhaa kutoka kwa Waalgeria.
Matokeo hayo yanaifanya Algeria kuongoza Kundi E baada ya kukusanya pointi sita, ikifuatiwa na Burkina Faso na Sudan zenye pointi tatu kila moja, huku Equatorial Guinea ikiwa haina pointi yoyote na hivyo kusukumwa nje ya mashindano hayo.
Mapema ya mapema ya kundi hilo, Sudan iliichapa Equatorial Guinea bao 1-0. Timu hizo nne zitakamilisha mechi za hatua ya makundi Jumatano, ambapo Algeria watacheza na Equatorial Guinea mjini Rabat na Burkina Faso itakikipiga na Sudan huko Casablanca.