Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Chelsea yamtaka John Stones

STONES Pict

Muktasari:

  • Mbali na Stones, Chelsea inaendelea na mazungumzo ya kumsajili beki wa Crystal Palace, Maxence Lacroix, huku pia ikimfuatilia beki wa Como, Jacobo Ramon, kama sehemu ya mpango wa kuimarisha safu ya ulinzi kabla ya kuanza kwa msimu mpya.

LONDON, ENGLAND: CHELSEA imeingia katika mbio za kumsajili beki wa kimataifa wa England, John Stones, kwa uhamisho wa bure baada ya mkataba wake na Manchester City kumalizika mwishoni mwa Juni.

The Blues sasa zinashindana na Inter Milan, ambayo pia inamuwania beki huyo mwenye umri wa miaka 32.

Mbali na Stones, Chelsea inaendelea na mazungumzo ya kumsajili beki wa Crystal Palace, Maxence Lacroix, huku pia ikimfuatilia beki wa Como, Jacobo Ramon, kama sehemu ya mpango wa kuimarisha safu ya ulinzi kabla ya kuanza kwa msimu mpya.

STON 01

Wapanga kuwauza mabeki

Ili kutoa nafasi kwa wachezaji wapya, Chelsea pia inatarajia kuwaachia baadhi ya mabeki wake.

Beki wa England, Trevoh Chalobah, yupo kwenye mazungumzo ya kuhamia Como, huku Axel Disasi na Benoit Badiashile wakitajwa kuwa miongoni mwa wachezaji waliowekwa sokoni.

STON 01 (1)

Stones ana historia kubwa City

Stones alijiunga na Manchester City akitokea Everton mwaka 2016 kwa ada ya pauni47.5 milioni na kucheza mechi 295 akiwa na mabingwa hao wa zamani wa Ligi Kuu England.

Katika kipindi chake Etihad, alitwaa mataji sita ya Ligi Kuu, Ligi ya Mabingwa Ulaya, FA Cup mara mbili, Kombe la Ligi mara tano, Ngao ya Jamii mara tatu, Kombe la Dunia la Klabu pamoja na UEFA Super Cup.

Akiwa na timu ya taifa ya England, Stones amecheza mechi 93 na alikuwa sehemu ya kikosi kilichomaliza katika nafasi ya tatu kwenye Kombe la Dunia 2026.

STON 03

Chelsea yaendelea kutikisa dirisha

Hatua ya kumuwania Stones inakuja siku chache baada ya Chelsea kutangaza rasmi usajili wa kiungo wa England, Morgan Rogers, kutoka Aston Villa kwa ada ya pauni milioni 117, ambayo ni rekodi mpya ya klabu.

Wakati huohuo, Chelsea inaendelea na mazungumzo na Aston Villa kuhusu uwezekano wa kumpeleka kwa mkopo winga wa Argentina, Alejandro Garnacho, kuelekea Villa Park.

Iwapo mazungumzo yatafanikiwa, Stones anaweza kuwa mmoja wa nyongeza muhimu katika kikosi cha Chelsea kinachojiandaa kupigania mataji msimu wa 2026-27.