Yanga yarudi kambi ya ushindi Dar
Mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC, Yanga wanaingia kambini Avic Town Kigamboni leo kwa ajili ya kujiandaa na michezo iliyobaki ya Ligi kuu na Kombe la Shirikisho la Azam.
Wachezaji wa timu hiyo wanatarajia kuwasili leo alasiri kambini ambapo watafanya mazoezi katika Uwanja wa Avic saa kumi kisha wataendelea na ratiba zao zingine .
Yanga imebakiwa na michezo mitatu ya Ligi kuu na mmoja wa fainali ya Kombe la Shirikisho Azam ambapo kwenye Ligi mchezo wao wa mwisho nyumbani watawakaribisha timu ya Polisi Tanzania utakaochezwa jumatano jijini Dar es Salaam kabla ya kuelekea jijini Mbeya kuwavaa Mbeya City huku wakitarajiwa kukabidhiwa kombe Lao katika mechi hiyo.