Yanga watamba CAF ni moto, kambi Morocco
Uongozi wa Yanga tayari umewapa mapumziko ya wiki mbili wachezaji wake kisha watakusanyika kwenda kambini Morocco mwanzoni mwa wiki ya pili mwezi ujao kujiandaa na msimu ujao.
Mshauri wa uongozi wa Yanga, Senzo Mazingiza akizungumza baada ya kurudi jijini Dar es Salaam wakitokea Kigoma alisema wachezaji wamepewa mapumziko wakaonane na familia.
“Wachezaji wanaenda kupumzika wakirudi tuwe na kazi ya kujiandaa na msimu ujao.”
Pia Senzo amesema wamejidhatiti na Yanga ijayo itakuwa imara zaidi na yenye uwezo wa kupambana Ligi ya Mabingwa Afrika inayoanza Septemba 11.
Mwanaspoti linafahamu sehemu kubwa ya kikosi Yanga kitaenda Morocco, lakini wachezaji wengine watabaki Dar kwa ajili ya Kombe la Kagame linaloanza Agosti, mwaka huu.