Wafanyakazi wa Hoteli ya Oakland’s Afrika Kusini wamlilia Kibonde
Muktasari:
Kibonde alikuwa akitumia hoteli hiyo pamoja na wenzake walipokuwa wakienda Afrika Kusini kwa shughuli za kikazi.
Wafanyakazi wa Hotel ya Oakland's Inn, Kitongoji cha Randburg, Johannesburg, Afrika Kusini wamemwelezea Mtangazaji maarufu Ephraim Kibonde jinsi walivyomfahamu wakati wa uhai wake.
Kibonde alikuwa akitumia hoteli hiyo pamoja na wenzake walipokuwa wakienda Afrika Kusini kwa shughuli za kikazi.
Wafanyakazi hao walikutana na Mwandishi wa MCL Digital, Edo Kumwembe na kuzungumza naye, huku wakionyesha hisia zao na kuwaombea familia yake kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo
Charity ambaye ni Meneja wa hoteli hiyo alizungumzia kwa namna walivyomfahamu Kibonde wakati akienda nchini humo kwa shughuli zake za kikazi.
Pia mfanyakazi mwingine wa hoteli hiyo, Bwana Hunter ambaye ni msimamizi wa hoteli alisema alimwelezea Kibonde kwa namna alivyomfahamu pia akiwaombea wanafamilia wake katika kipindi hiki kigumu.