Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Vunja Mbavu: Zaa-Hela: Soka la bongo bila Wema Sepetu haiwezekani

Muktasari:

Aliyekuwa kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera alitimuliwa na klabu hiyo wiki chache zilizopita baada ya kuifundisha kwa msimu mmoja na miezi mitatu ya msimu wa pili klabuni hapo.

Mwandishi: Haloo Papa Zaa-Hela, habari yako bana? Upo Dar, Kinshasa au Parii?
Zaa-Hela: Acha shobo wewe, kaanza habari zipi? Za kuishi kifahari Ufaransa? Au za kuja Tanzania kuwekeza kwenye ‘Akademyee ya Soka’?
Mwandishi: Yoyote. Kwanza wameshakulipa pesa yako?
Zaa-Hela: Kina nani? Kama ninhao mabeberu wa Jangwani hawana hela ya kunilipa. Labda mimi ndo niwakopeshe.Mwandishi: Umeona timu hivi sasa inashinda tu kwa pasi za kampa kampa tena. Siyo wewe na soka la kujilinda kama Masai.
Zaa-Hela: Kama mfungaji wao tegemeo nimemleta mimi, nani anapaswa kupongezwa?
Maana siyo unajisifu kuoa mke wakati anaishi kwa ubini wangu.
Mwandishi: Anayemfundisha kwa sasa. Wewe ulichokuwa unamuelekeza ni namna ya kutaua miguu na kutetemeka kabla ya kupiga faulo.
Zaa-Hela: Shubaamiti wewe... Kwanza vipi Wema Sepetu yupo? Nasikia toka niondoke anakondeana tu ndenge nini?
Mwandishi: Kwani wewe ulikuwa unampa nini? Au ulikuwa ‘sponsa’ wake?
Zaa-Hela: Yule ni fansi ya Yanga. Nilipoondoka yeye analiumua sana. Hakutaka kabisa niondoke tatizo watu wa Yanga hamjui mpira. Mnajua kelele tu.
Mwandishi: Nitake radhi mimi siyo Yanga. Halafu pili habari za Wema hazihusiani na soka.
Zaa-Hela: Tanzania bila Wema haiwezekani. Ile binti ukiitazama kwa pasii unajikuta hata jinsi ya kufundisha mpira unakosa ‘konsetreshoo’.
Mwandishi: Kwa hiyo yeye ndo alifanya uwe unajipangia timu kama nyumba vile unavaa pensi?
Zaa-Hela: Kwanza niambie nasikia kocha wa Simba naye wamemtimu?
Mwandishi: Sasa nitajuaje kama wamemtimua au katimka mwenyewe?
Zaa-Hela: Kwani.wewe si mwandishi? Na kazi ya mwandishi si kuchunguza? Au wewe unachunguza maisha yangu tu?
Mwandishi: Nachunguzaje wakati wewe mwenyewe unaropoka sana . Yaani huwezi kuweka pozi. Kabla hujapewa barua ya kuvunja mkataba ukaongea maneno mengi sana.
Zaa-Hela: Kwa hiyo wewe nini kinakuuma? Kwanza wewe ni mwanahabari gani hujui kama Kidefu Ndevu katimuliwa Simba?
Mwandishi: Hapa nashughulika na wewe acha kunitajia wasiokiwepo.
Zaa-Hela: Simba na Yanga kama minyoo. Hawaeleweki wapi mbele wapi nyuma. Mimi kudroo mechi moja kosa. Haya huyo wa Simba naye vipi anajilinda sana?
Mwandishi: Sasa wewe umekuwa mwandishi tayari unanibana na maswali?
Zaa-Hela: Nyinyi wambea tu mnasingizia mimi sijui fundisha mpira. Mkanitimua sasa huyo wa Simba naye kakosa nini? Ndo maana nasema hamjui mpira Tanzania.
Mwandishi: Wewe ulizidi bana, ulikuwa hata hujui kikosi gani cha kwanza na nani wa kumtoa na wakati gani.
Zaa-Hela: Acha ukuda ndezi wewe. Nilipokuwa nampanga kila siku Molinga mliona nampendelea. Sasa vipi hao waliobaki nao hawampangi?
Mwandishi: Unakuja lini Bongo? Simba kama kweli wamemtimua kocha si uje uchukue nafasi yake?
Zaa-Hela: Mimi siwezi fundisha timu yenye mtu tajiri zaidi yangu. Hata kule Zambia niliacha kwenda kufundisha kwa sababu kuna mtu alikuwa tajiri. Nilipoambiwa Yanga wanaishi kama yatima nikasema hapahapa.