Mosimane bye bye Al Ahly
Klabu ya Al Ahly ya nchini Misri imekubali ombi la kocha Pitso Mosimane la kutaka kuondoka baada ya mafanikio aliyopata na timu hiyo.
Katika kikao kilichokaa kimekubaliana kwa pande zote kuwa Mosimane ataacha kazi hiyo na wamemtakia kila la kheri.
Mosimane ameshinda mataji 5 tangu ajiunge na timu hiyo 2020 yakiwemo ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara 2, Egyptian Cup mara moja na Caf Super Cup mara mbili.
Kocha huyo raia wa Afrika Kusini katika mechi 97 ameshinda 65 sare 22 na akipoteza 10 ikiwemo ile ya Simba katika uwanja wa Mkapa.